Header Ads Widget

IGHALO AONGEZEWA MKATABA UNITED HADI JANUARI, 2021


                   Mshambuliaji wa Manchester United, Odion Ighalo


Na Damian Masyenene

Klabu ya Manchester United ya nchini Uingereza ‘Mashetani Wekundu’ imefikia makubaliano ya kuendelea kupata huduma ya mshambuliaji raia wa Nigeria, Odion Ighalo kwa kumuongezea mkataba hadi Januari 31, mwaka 2021.

Ighalo ambaye ni mchezaji wa timu ya Shanghai Shenhua ya China, yupo kwa mkopo katika klabu ya Manchester United tangu dirisha dogo mwanzoni mwa mwaka huu, ambapo mkataba wake huo wa mkopo ulitarajiwa kukoma Mei 31, 2020 (mwisho wa msimu) kabla ya kuvurugwa na janga la Corona.

Kwa mujibuwa taarifa zilizochapishwa na kituo cha Sky Sport cha Uingereza, Mnaijeria huyo ambaye ameichezea United michezo nane katika mashindano yote na kufunga mabao manne, anatarajiwa kusaini mkataba mpya na klabu yake ya Shanghai Shenhua utakaodumu hadi 2024 wenye thamani ya Euro 4000 kwa wiki.

Ighalo alijiunga na United kwa mkataba wa muda mfupi katika siku ya kufunga dirisha dogo la usajili Januari mwaka huu, ambapo lilikuwa chaguo la Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Ole Gunnar Solskjaer kupata suluhisho la safu ya ushambuliaji kufuatia mshambuliaji tegemeo, Marcus Rashford kupata majeraha ya mgongo mwishoni mwa mwaka jana