Header Ads Widget

MWANAMKE ASAKWA NA POLISI SHINYANGA KWA KUTELEKEZA MTOTO WA SIKU 2.


                  
                    Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga ACP Debora Magiligimba. 

Na Suzy Luhende-Shinyanga  

Jeshi la polisi Mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo ya Kijiji cha Mwakitolyo linamtafuta Mwanamke  mmoja ambaye bado hajafahamika jina wala makazi yake kwa kosa la kumtupa mtoto mchanga.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga  ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo limetokea May  19 Mwaka huu majira ya saa mbili asubuhi huko katika kitongoji cha Mwakitolyo namba 5  kijiji cha Mwakitolyo tarafa ya Nindo halmashauri ya  Shinyanga vijijini mkoani hapa.

Kamanda Magiligimba amesema kuwa mtoto asiyejulikana jina jinsia ya kiume na anayekadiliwa kuwa na umri wa siku mbili tangu kuzaliwa kwake amekutwa akiwa ametupwa na kutelekezwa kichakani na mama yake mzazi ambaye bado hajafahamika.

 Aidha mtoto huyo mchanga amekutwa akiwa amevilingishwa kwenye Kanga ambapo  tayari amepelekwa Zahanati ya Kijiji cha Mwakitolyo na kupewa huduma ya kwanza na hali yake inaendelea vizuri chini ya uangalizi wa karibu zaidi wa watalaaamu wa huduma ya afya.

Aidha Kamanda wa Polisi Mkoani Shinyanga ametoa rai kwa wakazi wa mkoa huo hususani maeneo ya Wachimbaji wa Madini ya Dhahabu  kuendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha kukamatwa kwa Mtuhumiwa huyo ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake.