Header Ads Widget

TAFORI YABAINI AINA 10 ZA MITI INAYOWEZA KUFUBAZA CORONA

 Mhifadhi Mkuu wa Msitu wa Hashi Lubaga Manispaa ya Shinyanga Ramadhan Mzirayi akionesha aina mbalimbali ya miti iliyopo ndani ya msitu huo ambayo inatibu magonjwa mbalimbali.
-------------
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI)Dkt. Revocatus Mushumbusi amesema wamebaini aina kumi za miti ambayo inauwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali ikiwemo kufubaza dalili za awali za ugonjwa wa homa kali ya mapafu COVID 19.


 Kaimu Mkuu wa Kanda ya ziwa wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania(TAFORI) Iddy Dibwa akionyesha aina ya miti iliyopandwa ambayo tayari imefanyiwa utafiti.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI Dkt. Revocatus Mushumbusi akizungumza na waandishi wa habari katika hifadhi ya misitu Hashi Lubaga Manispaa ya Shinyanga.ambapo amesema kuna miti kumi ya dawa za asili ambayo ni bora zaidi na inatumika sana mikoa ya kanda ya ziwa.
 Mtaalamu wa tiba mbadala Mussa Kuhangaika akieleza jinsi dawa za asili zinavyofanya kazi ikiwemo kutibu magonjwa mbalimbali.


Na mwandishi wetu 
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI)Dkt. Revocatus Mushumbusi amesema wamebaini aina kumi za miti ambayo inauwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali ikiwemo kufubaza dalili za awali za ugonjwa wa homa kali ya mapafu COVID 19.

 Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara yake ya  kutembelea hifadhi ya misitu ya asili Hashi eneo la Lubaga Manispaa ya Shinyanga,ambapo shughuli za utafiti na uoteshaji wa miti zinafanyika amesema miongoni mwa majaribio yaliyoanzishwa na kusimamiwa kwa uangalifu na taasisi hiyo ni pamoja na jaribio la mti ya dawa ya asili.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAFORI alisema kupitia utafiti huo waligundua miti ya dawa ya asili takribani  300 inayotumika kutibu zaidi ya magonjwa 100 na walipoifanyia uchambuzi miti 10  ilikuwa bora zaidi kutokana na kutumika mara kwa mara kanda ya ziwa.

“Aina ya miti hiyo  ni Mlungulungu ambayo mizizi na majani yake yanatibu homa na madonda kwa kujifukiza,Nengonengo inatibu athma(kushindwa kupumua)ikiwa ni miongoni mwa dalili za Corona,Mzima unatibu homa kali na Mwatya/mkalya inatibu magonjwa ya ganzi ya mwili,kichwa namatatizo ya tumbo.”amesema Kaimu Mkurugenzi.

Miti mingine ni Mlundalunda unatibu matatizo ya tumbo,kifua,ngili,ganzi ya mwili,mti wa Mfutwambula/ng’wengwambula matatizo ya tumbo,kifua,athma na ngili,mti wa Msana unatibu mapafu,kikohozi,vidonda vya kooni na miti ya Mondo,Mgada na Ningiwe yote inatibu matatizo ya presha,tumbo na ganzi.

 Kutokana na janga la ugonjwa wa Corona ambalo mpaka sasa halijapata chanjo wala tiba,mtaalamu wa tiba za asili na muuzaji wa madawa Mussa Kuhangaika mkazi wa Shinyanga,aliomba wizara ya afya Kuwashirikisha wataalamu wa tiba mbadala ili kuweza kupata dawa ya aina moja inayotibu Corona.

Naye Kaimu Mkuu wa TAFORI kanda ya ziwa Iddy Dibwa amesema  miti ni chanzo kikuu cha dawa za asili zinazotumiwa na wananchi wengi kutibu magonjwa mbalimbali kanda ya ziwa na utafiti huo wamefanya ili kutambua dawa za miti shamba zinazotumika sana kanda hiyo.
Mwisho.