Header Ads Widget

ASKOFU MABUSHI: TAMKO LA JPM SI LA KUKURUPUKA

 Askofu wa Kanisa la IEAGT la mjini Shnyanga, David Mabushi



Na Mwandishi wetu

Askofu wa Kanisa la International Evangelical Assembly of God Tanzania (IEAGT) la mjini Shinyanga, David Mabushi amesema kuwa tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli kuruhusu shughuli mbalimbali nchini kurejea katika hali ya kawaida ifikapo Juni mosi, mwaka huu siyo ya kukurupuka na hailipeleki taifa katika moto wa ugonjwa wa Corona.


Mei 21, mwaka huu Rais Magufuli alilitangazia taifa kuwa shughuli mbalimbali yakiwemo masomo ya vyuo na kidato cha sita pamoja na michezo ya ligi kuu, daraja la kwanza na la pili vitarejea ifikapo Juni Mosi, mwaka huu baada ya kusimama kwa takribani miezi miwili kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona.

Ambapo kufuatia tamko hilo, Askofu Mabushi akizungumza na waumini wake leo katika ibada ya ijumaa amewataka kusherekea tamko hilo kwa kuwa ni ishara ya kupungua kwa maambukizi ya ugonjwa wa Corona  kutokana na maombi ambayo Mungu amejibu kwa taifa letu.

Mabushi amesema kuwa Rais Dk. Magufuli hajakurupuka kwa tamko alilolitoa jana kwani amefanya utafiti wa kutosha na amejua ukweli halisi wa hali ilivyo kwa kupata taarifa mbalimbali kutoka kwa watendaji wake.

“Naamini kuwa Rais na Serikali yake hawezi kukubali kuliingiza taifa katika moto mkubwa wa Corona kama hana mapenzi na wananchi wake,” alisema Askofu Mabushi.

Kwa upande mwingine Askofu Mabushi aliwaomba waumini wa kanisa hilo kufanya maombi ya kumshurukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa amejibu maombi ambayo waliomba tangu mwanzo wa janga hilo kuripotiwa na kupelekea Serikali kufunga baadhi ya shughuli zenye mikusanyiko ya watu na kuacha uhuru wa nyumba za ibada kuendelea kumcha Mungu ili kuvusha taifa katika vita ya ugonjwa huo.

Pia amewaasa wanafunzi kwenda kuongeza jitihada zaidi ya masomo yao pindi watakaporudi mashuleni ili kukamilisha malengo yao ya kimasomo na wasome bila hofu na kujikita zaidi katika kufata kanuni za afya na usafi ili wakamilishe masomo yao kwa amani.