` UPANUZI WA VYUO VYA VETA: MKAKATI WA SERIKALI UTAKAVYOFUTA CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA AJIRA

WANDAMAN HOTEL

UPANUZI WA VYUO VYA VETA: MKAKATI WA SERIKALI UTAKAVYOFUTA CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA AJIRA

Na Mwandishi Wetu

Uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika kupanua elimu ya ufundi stadi nchini unatajwa kuwa mwarobaini utakaomaliza kabisa changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana na kuwazika katika shughuli za uzalishaji mali, kupitia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya vyuo vya VETA. 

Hatua hii itawawezesha vijana wengi kote nchini kupata ujuzi wa vitendo utakaowaondoa vijiweni na kuwapa fursa ya kujiajiri au kuajiriwa kwa urahisi. 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidhi Ameir, aliliambia bunge kuwa mkakati huo unatekelezwa kupitia Mradi wa Pili wa Elimu na Ujuzi kwa Ajira Zenye Tija (ESPJ II), unaolenga kuwabadilisha vijana kuwa nguvu kazi yenye tija na yenye shughuli za kufanya muda wote.

Katika kuhakikisha vijana maeneo ya vijijini wanajazwa ujuzi na kuwa 'bize' na kazi, serikali imetenga shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya kukarabati Chuo cha VETA Ulyankulu mkoani Tabora. 

Akijibu swali la Mbunge wa Ulyankulu, Japhael Lufungija, Naibu Waziri Wanu alieleza kuwa kazi za awali zikiwemo za majengo ya utawala na karakana zimeshakamilika kwa asilimia 93.5, hatua itakayofungua milango kwa vijana wengi wa eneo hilo kupata ujuzi utakaowaingiza moja kwa moja kwenye sekta ya uzalishaji na kuachana na utepetevu.

Wakati huo huo, mkakati huo unaenda sambamba na ukamilishaji wa Chuo cha VETA Wilaya ya Kigamboni mwezi Agosti 2026, ambacho kitakuwa kimbilio la vijana wa Dar es Salaam wanaosaka ujuzi utakaowaondoa kwenye utegemezi. 

Akijibu swali la Mbunge wa Kigamboni, Faustine Ndugulile (aliyetajwa kama Haran Sanga bungeni), Wanu alisema serikali imetenga shilingi bilioni 2.34 kwa ajili ya vifaa vya mafunzo nchi nzima, ambapo shilingi milioni 36 zitaenda Kigamboni ili vijana wakute kila kitu tayari, jambo litakalowapa motisha ya kujikita kwenye masomo ya ufundi na hatimaye kuanzisha karakana na biashara zao.

Ujenzi huu wa Kigamboni ni sehemu ya mpango kabambe wa serikali wa kujenga vyuo 65 vya VETA katika wilaya 64 pamoja na Mkoa wa Songwe, maeneo ambayo hapo awali yalikuwa hayana fursa hizo. 

Kusogezwa huku kwa vyuo vya ufundi katika ngazi ya wilaya kunatarajiwa kubadilisha kabisa mtindo wa maisha ya vijana nchini, kwani kutawapa mazingira ya kujifunza kazi za mikono, kuwatoa kwenye wimbi la uhalifu na unyanyasaji, na badala yake kuwapa maisha mapya yenye misingi imara ya kiuchumi kupitia ajira za uhakika.

[11:45, 18/06/2026] TBN Beda: Haja ya Utulivu, Demokrasia na Amani Katika Kufanikisha Mchakato Endelevu wa Katiba Mpya Nchini

Serikali imesisitiza kuwa mchakato wa kupata Katiba Mpya unahitaji utulivu wa kisiasa, amani, na misingi thabiti ya kidemokrasia ili uweze kutekelezwa kwa tija, ikibainisha kuwa jambo hilo litafanyika wakati mwafaka kulingana na taratibu zilizowekwa. 

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa sheria mama ya nchi inatokana na mahitaji mapana ya Watanzania wote na si matakwa ya kundi fulani au chama kimoja cha siasa. 

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Juma Homera, alieleza hayo wakati akifafanua msimamo wa serikali kufuatia hatua ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutangaza kamati ya kuanza mchakato huo ndani ya siku 90, akihimiza umuhimu wa wananchi kuwa na subira wakati serikali ikitekeleza mpango huo kwa utulivu ndani ya ratiba yake ya miaka mitano.

Dk. Homera alisema kuwa Tanzania ni nchi inayozingatia uhuru wa kutoa maoni na kwamba makundi yote yana haki ya kuchangia mawazo yao kuhusu masuala ya kitaifa, mradi tu wafanye hivyo kwa kufuata sheria ili kulinda amani iliyopo. 

Alibainisha kuwa suala la Katiba Mpya limeainishwa wazi katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na limekuwa likizungumzwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ikiwa ni pamoja na kugusiwa kwenye mapendekezo ya Tume Huru ya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Hii inaonesha kuwa dhamira ya serikali ipo palepale, lakini inahitaji mazingira yenye utulivu ili kufanya maamuzi sahihi ya kikatiba kwa maslahi ya taifa zima.

Wakati serikali ikihimiza mwelekeo huo wa kisheria na utulivu, Chadema kupitia Katibu Mkuu wake, John Mnyika, imetangaza kamati ya wajumbe 11 itakayoongozwa na Mwenyekiti Dk. Rugemeleza Nshara na Katibu Deogratius Mainyira, ikiwa na jukumu la kuandaa mkakati na rasimu ya muswada wa kukwamua mchakato huo kabla ya mwaka 2027. 

Kamati hiyo, inayohusisha pia wataalamu washauri wasio wanachama wa chama hicho, imepanga kukutana na asasi za kiraia, taasisi za dini, na wadau mbalimbali ili kukusanya maoni. 

Muktadha huu mzima wa kisheria na kisiasa unaonesha kuwa, ingawa kuna shauku kubwa ya mabadiliko ya kikatiba, ustawi wa demokrasia na uhifadhi wa amani ya nchi bado ndio nguzo kuu zitakazowezesha utekelezaji wa Katiba Mpya bila kutikisa misingi ya taifa.

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464