` KATIBU MKUU JUMUIYA YA WAZAZI CCM TAIFA ASAKA KURA ZA RAIS VIJIJINI,AWAOMBA WANANCHI KUKIPA RIDHAA TENA OCTOBA 29

KATIBU MKUU JUMUIYA YA WAZAZI CCM TAIFA ASAKA KURA ZA RAIS VIJIJINI,AWAOMBA WANANCHI KUKIPA RIDHAA TENA OCTOBA 29


Katibu Mkuu Jumuiya ya wazazi CCM Taifa Ally Hapi akizungumza na wakazi wa Kata ya Mwamala Jimbo la Itwangi wakati akiomba kura za Mgombea urais Dk Samia Suluhu Hassan na wagombea wa Ubunge na Udiwani wa chama hicho.


     Katibu wa Jumuiya ya wazazi Mkoa wa Shinyanga Regina Ndulu akisalimiana na Katibu Mkuu wa Juumuiya ya wazazi Taifa Ally Hapi mara baada ya kuwasili Mkoani Shinyanga kusaka kura za mgombea Uraisi Dk Samia Suluhu Hassan

Suzy Butondo, Shinyanga 

Katibu mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapi  amefanya  ziara mkoani  Shinyanga ya kuhamasisha wananchi wajitokeze kupiga kura oktoba 29 mwaka huu,ambapo amewaomba wampigie kura  mgombea Urais wa CCM  Samia Suluhu,wabunge na madiwani wote wa Chama hicho, 

 

Hayo ameyasema  wakati  akizungumza na wananchi wa jimbo la Itwangi  Mkoani Shinyanga, amesema Chama Cha mapinduzi CCM kwa kusimamiwa na Rais Samia Suluhu imejipanga  vizuri kuhakikisha  iinainua maisha ya kila mtanzania, hivyo amewaomba kuwapa ridhaa tena.

 

Hapi  amesema ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM iliyopita   imetekelezwa kikamilifu , lakini ilani ya sasa imesheheni mambo makubwa zaidi  kuliko ilani iliyopita kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, ili kuhakikisha kila mmoja anainuka kiuchumi.

 

"Niwaombe sana wananchi wa mkoa wa Shinyanga mjitokeze wote kupiga kura mkipigie chama cha Mapinduzi CCM kwa sababu kimesimamia ilani ya CCM,na awamu hii ilani  yetu imesheheni mipango mikubwa na tunasema ilani hii kama ni Ng"ombe ni Nzagamba,"amesema Hapi


                                             
                                           Mapokezi yanaendelea

         Amesema CCM imefanya mabadiliko makubwa kulikuwa hakuna umeme lakini kwa sasa   kila kijiji kina umeme, maji ilikuwa ni shida lakini kwa sasa kila kijiji kina maji bado vitongoji vichache ambavyo hadi kufikia 2030 vitakuwa vimefikiwa.

 

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John Siagi amewaomba wananchi wote wajitokeze kupiga kura ili wakichague chama cha Mapinduzi kwa sababu kina ilani iliyosheni mipango ya kuwasaidia wananchi ili waweze kujikwamua kiuchumi.

 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa ameongozana na timu yake ambapo amefanya mikutano katika Kata ya Samuye, Mwamala, Usule kisha baadhi ya viongozi wa Jumuiya hiyo kumwakilisha kutano wa Tinde baada ya kupata dharura ya kikazi.



           Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John Siagi akizungumza na wananchi wa Kata ya Mwamala Jimbo la Itwangi ambapo amewaomba kuwapa kura wagombea wa chama hicho Rais,ubunge na udiwani

  Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Edward Ngelela akiomba kura



  Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi  CCM Wilaya ya Shinyanga Vijijini  Fadhili Naftari akisalimiana na wananchi wa Kata ya Mwamala wakati wa kuomba kura za Rais,wagombea ubunge na udiwani




                     Baadhi ya viongozi kutoka Jumuiya ya wazazi Taifa wakiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Ally Hapi wakiomba kura kwa wananchi wakichague chama cha Mapinduzi.

      Baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya wazazi 






 

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464