
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Mrindoko amewaomba waendesha boda boda, wajasiliamali, mama lishe wanachama na wananchi wote wa kata ya Kitangili wajitokeze kwa wingi kwa ajili ya kuwapigia kura wagombea wa CCM Rais Samia Suluhu, mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Patrobas Katambi na diwani wa kata ya ya Kitangili Jonathan Madete ili wapate kura za kishindo.
"Chama cha mapinduzi CCM kimefanya maendeleo makubwa katika kata yetu hii ya Kitangili na Taifa kwa ujumla tunayaona kwa macho kila sekta hatusubiri kuambiwa, hivyo tunatakiwa tujitokeze wote tukawapigie kura wagombea wetu wa CCM ili waendelee kufanya makubwa zaidi"Mrindoko
Katibu wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Shinyanga Doris Kibabi amesema wamefanya ziara hiyo kwa lengo la kuhamasisha wanachama wananchi wote wa Kitangili wajitokeze kupiga kura, asitokee hata mmoja ambaye atapata udhuru siku hiyo wa kwenda kupiga kura.
Kwa upande wake mgombea udiwani kata ya Kitangili Jonathan Madete amewaomba wananchi, wajasiliamali boda boda, na mama lishe wampigie kura nyingi za kishindo mgombea Urais wa CCM, mbunge na yeye diwani ili watakaposhinda waweze kuleta mabadiliko na kushirikiana nao ili kuwapatia mikopo yenye riba nafuu ili kila mmoja ajikwamue kiuchumi.
mjasiliamali.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Shinyanga Fue Mrindoko akizungumza na waendesha bodaboda viongozi wa timu za mpira wajasiliamali wa mbogamboga na mama lishe
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Shinyanga mjini Doris Kibabi akizungumza na waendesha bodaboda viongozi wa timu za mpira wajasiliamali wa mbogamboga na mama lishe
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Shinyanga mjini Doris Kibabi akitoa maelekezo ya kupigia kura wagombea kwa waendesha bodaboda viongozi wa timu za mpira wajasiliamali wa mbogamboga na mama lishe
Mgombea Udiwani kata ya Kitangili Jonathan Madete akizungumza na wananchi wa kata hiyo
Mgombea Udiwani kata ya Kitangili Jonathan Madete akizungumza na wananchi wa kata hiyo
Mratibu wa kata ya Kitangili Mwajuma Rabia akizungumza na wananchi wa kata ya Kitangili
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464