

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga leo Septemba
29,2025 limezindua rasmi Kimkoa Kampeni ya Tuwaam bie mapema kabla
hawajaharibiwa katika Wilaya ya kipolisi Ushetu ,kwa lengo la kuwalinda watoto
kutimiza ndoto zao.
Akizindua
Kampeni hiyo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga Janeth Magomi amesema
huo ni mpango mahususi unaosimamiwa na kitengo cha Dawati la jinsia na watoto ili
kuongeza uelewa kwa Jamii.
Amesema
kampeni hiyo inalenga kujenga Jamii yenye misingi ya heshima,usalama na ulinzi
wa mtoto kwa kuwawezesha kutimiza ndoto zao na siyo kujiunga na makundia ambayo
hayana tija na yanaweza kuwaharibia mwelekeo.

Amesema wamelenga kuondoa au kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuielimisha jammii kutambua kuwa vitendo vya udhalilishaji ni kosa la jinai na kuripoti ili kuchukuwa hatua za kisheria.



.jpeg)
.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464
.jpeg)