

WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA WAJENGEWA UWEZO
NA EUNICE KANUMBA SHINYANGA
IKIWA ni maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi October mwaka 2025, jumla ya wasimamizi wasaidizi 34 wa ngazi ya kata jimbo la Shinyanga wamejengewa uwezo leo tarehe 4 August lengo likiwa ni kusimamia uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 october 2025 kwa weledi.
Akizungumza wakati wa ufungunzi wa mafunzo hayo msimamizi wa uchaguzi jimbo la Shinyanga mjini Ally Lihuye amewataka watendaji hao kufuata sheria na taratibu na miongozo ya tume hiyo pasipo kuwajibuika kwa mamlaka nyingine kwani tangu walipoteuliwa kwa ajili ya utekelezaji wa jukumu hilo wamekuwa ni watumishi wa muda wa tume huru ya uchaguzi .
“Tume iliwaridhia wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya kata kutekeleza kazi za uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo uteuzi wenu umezingatia masharti ya kifungu cha sita(1),(2) na 5 na kifungu cha nane ( 1) na( 2) vya Sheria ya Uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani”amesema Lihuye
Lihuye pia amewashihi watendaji hao kujiepusha kuwa vyanzo vya malalamiko utoka kwa vyama vya siasa na wadau wa uchaguzi pia wahakikishe wanazingatia ipasavyo katiba ,shera,kanuni ,miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na tumen a kuanisha kuwa vyama vyote vya siasa vilivyo na usajili vishirikishwe kwa ukamilifu kwa hatua zote kwa kuzingatia matakwa ya katika,sheria,kanuni na maelekezo.
Katika hatua nyingine wasimamizi wasaidizi hao 34 katika ngazi ya kata leo wamekula kiapo cha kujitoa kwa muda katika ushiriki wa chama chochote cha siasa pamoja na kutunza siri zitokanazo na mchakato wa uchaguzi kiapo kilichosimamiwa na Agness Mlimbi ambaye ni hakimu mkazi wa mahakama hakimu mfawidhi katika ngazi ya wilaya.





.jpg)
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464