` MAOMBI YA TUNDU LISSU YATUPILIWA MBALI

MAOMBI YA TUNDU LISSU YATUPILIWA MBALI


Maombi ya Lissu yametupiliwa mbali
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu.

Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya mapitio yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu kwa sababu ameyawasilisha kinyume cha sheria.

Lissu aliwasilisha maombi hayo akitaka Mahakama hiyo iitishe jalada la kesi ya tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo dhidi yake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam ili ilipitie na kuchambue mwenendo wa kesi hiyo wa Juni 2,2025.

Aliwasilisha maombi hayo akipinga kuahirishwa huko akidai kuwa hakukuwa na sababu za msingi za kuahirisha kutokana tu na sababu ya upande wa Jamhuri kuomba ahirisho kwa sababu walikuwa wamewasilisha maombi ya kuomba baaadhi ya mashahidi wao kufichwa.

Lissu aliwasilisha mahakamani hapo sababu sita za mapitio, ambapo jopo la mawakili wa Serikali likiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu Nassoro Katuga lilipinga maombi hayo kwa kuwasilisha pingamizi tatu kwa madai kuwa yaliwasilishwa kinyume cha sheria.

SOMA ZAIDI CHANZO NIPASHE

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464