Tatizo siolewi licha kupata mwanaume wenye fedha nyingi!
Ni jambo la ajabu sana pale mwanamke anapomaliza mwezi mzima hajapata mwanaume yoyote aliyemtongoza, mwanamke kutongozwa ni jambo zuri, mwenyewe anajikubali kuwa yeye ni mzuri ila usipotongozwa anajua hana mvuto.

Nasema hivyo kwa sababu sisi kina mama kabla hatujatoka ndani ni lazima tujitazame kwenye kioo, ila siyo kila anayekutongoza unamkubalia ila kutongozwa ni jambo muhimu kwetu kina mama.