` WAZAZI SHINYANGA WASHAURIWA KUWA MAKINI NA TEKNOLOJIA JUU YA MAELZI NA MAKUZI YA WATOTO

WAZAZI SHINYANGA WASHAURIWA KUWA MAKINI NA TEKNOLOJIA JUU YA MAELZI NA MAKUZI YA WATOTO

 



Na Kareny   Masasy

WADAU   Mkoani Shinyanga wameeleza  teknolojia ya habari iliyoingia  duniani  inatakiwa wazazi wawe makini katika suala la malezi na makuzi ya watoto wao  hasa matumizi ya mitandao ya kijamii na luninga kwa kuangalia vipindi  ambavyo vitaweza kuwajenga kimadili.

Hayo yamesemwa leo Mei,2025 kwenye mjadala uliokuwa unahusu Nafasi ya wazazi na walezi katika matunzo ya watoto   ambapo Afisa ustawi wa Jamii  Mkoa wa Shinyanga Lyidia Kwesigabo amesema  kila mwaka mwezi Mei, Tanzania ina adhimisha siku ya familia duniani ambapo kwa mwaka huu  kauli mbiu  inasema Mtoto ni Malezi ;Msingi  wa familia bora Taifa imara.

Mgeni rasmi katika mjadala huo Kaimu katibu tawala mkoa wa Shinyanga David   Lyamogi amesema  familia zilizopitia malezi bora hazina changamoto kubwa katika malezi yao pindi wakiwa wakubwa hivyo jamii inatakiwa ifahamu Malezi ya watoto ni muhimu yanaanzia pindi mama akiwa mjamzito.

Kwesigabo amesema majadiliano yote yaliyotolewa na wadau  yatafanyiwa kazi huku maadhimio yaliyotolewa kukutana mara kwa mara ili kuweza kujengana kimawazo na kuimarisha hali ya malezi ya watoto kwenye familia katika mkoa huu.

Afisa  Miradi kutoka Shirika la Invest in Children Society (ICS), Lucy Maganga amesema kuna aina tofauti tofauti  ya familia  ambapo kuna familia ya mama na watoto,baba na mama na watoto, wanafamilia wanaoishi na watoto   na majirani wote wanajumuishwa katika malezi na kutoka mchango ulio chanya kwa watoto.

Maganga amesema  watu  kwa pamoja wanaweza kumfundisha mtoto  mila na desturi nzuri ,maadili mema na stadi mbalimbali ili mtoto aweze kukua   bila kuwatenga kwa kuangalia jinsia zao.

Maganga  anasema hakuna familia isiyokuwa na changamoto hivyo lazima kuwepo na mawasiliano chanya kwa kila mmoja ili watu wote wajione kuwa ni sehemu ya familia ili waweze kumpa malezi bora mtoto.

Mwandishi wa habari  Anikazi Kumbemba  akiwakilisha Mada kwa niaba ya klabu ya waandishi wa habari (SPC) amesema  waandishi wa habari ni chachu ya  kuleta elimu  kwenye jamii juu ya teknolojia  inayoingia duniani kwani mataifa ya nje tayari yamekuwa yakitumia teknolojia habari kwa watoto wao.

Mwenyekiti wa watu wenye ulemavu   wa ngozi  mkoani Shinyanga na Mjumbe wa Shirikisho la watu wenye ulemavu  (Shivyawata) Unice Manumbu amesema  wapo wanawake  wanaopewa ujauzito na kukimbiwa wanapojifungua na wanalazimika  kwenda mitaani kuomba sababu  ya kukosa matunzo  na kuwafanya watoto ndiyo chanzo cha mapato.

Mwenyekiti  wa Umoja wa vituo vya kulelea watoto mchana  Damari Mollel  amesema  wao wamekuwa ndiyo walezi wakubwa watoto wazazi wako bize na shughuli  zao wakumbuke wanapo muachia msichana wa kazi mtoto ndiyo  anakuwa na mawazo aliyofundishwa  msichana huyo   awe na tabia nzuri au mbaya.

Mwenyekiti wa baraza la watoto Taifa Rafael Charles  amesema   mtoto akilelewa vizuri katika malezi yanayotakiwa  hata kushiriki kwenye  masuala mbalimbali ya kijamii  atakapo kuwa mkubwa ataweza kutoa  mchango wake  kulijenga taifa.

“Naishukuru serikali  katika utoaji wa  maoni katika dira ya maendeleo ya taifa walishirikisha kundi la watoto na Programu Jumuishi  ya Malezi na Makuzi na Maendeleo ya Awali ya  Mtoto  yamefikia   katika ngazi ya Halmashauri na kata kwa kuhakikisha mtoto anapata malezi yaliyobora na sahihi”amesema Charles.

Mwenyekiti wa baraza la  wazee Manispaa ya Shinyanga Stephano Tano amesema  suala la watoto kwenye malezi kuanzia  umri wa mwaka sifuri hadi minane wanaotakiwa kupata malezi bora  hivyo wazee nao wamekaa na kutathimini mmomonyoko wa maadili na kupinga ukatili wa wanawake na watoto hasa mambo ya lishe.

















 

MWISHO.


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464