Na Kareny Masasy,Shinyanga
MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga wamepongeza serikali kuchukua hatua kutekeleza miradi kwenye sekta mbalimbali huku wakitaka wataalamu kuendelea kutekeleza maazimio ya kwenye vikao.
Pia wameomba
miundombinu ya barabara iendelee
kuboreshwa zaidi ili wananchi
wanapokwenda kwenye shughuli zao na wafanyabiashara wasiweze kukwamishwa.
Madiwani hao
wamesema hayo leo tarehe 29/04/2025
kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani ambapo walieleza maazimio ya baraza lililopita walitaka miradi
iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ikamilike.
Diwani wa
kata ya Mwamala Hamis Maganga amesema
shule ya msingi Bugogo ilikuwa na hali
mbaya kuta zilikuwa na nyufa lakini
serikali imetoa fedha kujenga vyumba vya
madarasa viwili na ofisi moja na wanafunzi sasa wanasoma wakiwa kwenye mazingira mazuri.
Diwani wa
kata ya Iselamagazi Isack Sengerema
amesema kuna barabara ipo katika
kitongoji cha Mwabundala kuna mto ambapo linahitajika daraja ili wananchi waweze
kuvuka ameiomba Wakala wa barabara mjini na Vijijini (Tarura) kuhakikisha wanafanya matengenezo haraka.
Diwani wa kata ya Didia Masele Luhende amesema miundombinu ya barabara
kutoka Didia Lohumbo kwenda Solwa
inachangamoto wafanyabiashara wanashindwa kufika kwenye eneo la mashine
kufuata mazao ya biashara.
Makamu Mwenyekiti
wa Halmashauri hiyo Samson Nicodemas amewataka wataalamu waendele kufanyia kazi
maagizo yanayotolewa kwenye vikao nakuyafanyia kazi.
Kaimu Mkurugenzi
wa Halmashauri hiyo Sterwat Makali amesema baadhi ya shule zilitembelewa na
viongozi kutoka TAMISEMI ambapo shule ya msingi Bugogo tayari imeletewa fedha
shilingi Milioni 52 na vyumba viwili na
ofisi ya walimu vimekamilika.
Naye Meneja
wa Tarura wilaya ya Shinyanga Samson Pamphili amesema barabara ya kutoka didia kwenda Solwa yenye urefu wa kilomita 14 inafanyiwa
kazi na tayari kilomita 6 imechongwa na mkandarasi anasubiri malipo yake huku barabara ya kutoka
Tinde kwenda Usule ipo kwenye mpango wa fedha za dharura.
“ Kwa Ujumla Halmashauri ya wilaya ya
Shinyanga barabara zinazopitika vizuri ni asilimia 64.23 ambazo ziko kwenye kiwango cha wastani ni asilimia
18.75 na asilimia 17.01 ziko kwenye hali
mbaya” amesema Pamphil.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464