Header Ads Widget

MSANII HI SPEED KUTOKA NIGERIA AACHIA ZAWADI YA ALBUM KWA MASHABIKI


Precious Gift ni album mpya na ya kwanza kutoka kwa msanii wa muziki wa Afro Beat na Hiphop kutoka nchini Nigeria ambaye anafahamika zaidi kwa jina la Hi Speed.

Album ya Hi Speed ina nyimbo 13 ndani yake akiwa ameshirikiana na Mr Raw, Terry Akpala, Seriki, Halima Alao, Jumabee, Shatta Michy , Dj Baddoo, Jesse Jagz, Jay Teaser, Mf Honcho, Di’ja, Eche Ozoku, Dreez, Jahjah, Sharon Sonia, Yonique, Young J, Don Flash, Hajj, Itabreez na Zurezoo.
Lakini pia katika album hii iitwayo Precious Gift imeandaliwa na kuyarishwa na watayarishaji  mbalimbali kutoka nchini Nigeria ambao wamefanikiwa kufanya vizuri kazi mbali mbali akiwemo Mix Monster  pamoja na Don Adah.

Album hii inapatikana katika mitandao yote ya kusikiliza na kupakua muziki unaweza pia kumfuatilia kupitia ukurasa wake wa Instagram @hispeedmusic

Post a Comment

0 Comments