Header Ads Widget

MAAFISA MIFUGO WA KISHAPU,MSALALA,USHETU NA SHINYANGA VIJIJINI WAPATIWA PIKIPIKI

 

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,Sophia Mjema akikabidhi pikipiki kwa maofisa wa mifugo kutoka halmashauri nne za Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa shughuli zao.

 Maaofisa Mifugo kutoka Halmashauri nne za Mkoa wa Shinyanga wakiwa wakipokea pikipiki kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

 Na Kareny  Masasy

MKUU wa mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema amekabidhi pikipiki 12 kwa maafisa mifugo wa halmashauri nne  lengo kuwarahisishia kufika kwenye maeneo ya  wafugaji walio pembezoni  nakujua changamoto zinazo wakabili  na sio kwenda kuzibebea abiria nakufanya biashara.

Kila halmashauri itapata pikipiki  tatu ambazo ni  Kishapu,Msalala,Ushetu na Shinyanga vijijini.

Mjema  amesema  hayo jana wakati akikabidhi pikipiki hizo  kwa maafisa mifugo hao huku akieleza kuwa serikali   imeliona suala la changamoto na haitaki kusikia malalamiko kutoka kwa wafugaji kuwa hawajatembelewa wakati usafiri wamepata.

Ni suala la kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kutukumbuka na kutuondolea changamoto moja kwa nyingine  nasi tunasema hatuta muangusha katika utekelezaji wa kuwatumikia wananchi kwani pikipiki hizi zifanye kazi yake iliyokusudiwa sio kuzifanya bodaboda”.amesema Mjema.

Ofisa mifugo mkoa wa Shinyanga  Dioniz Gutav amesema kuwa pikipiki 12 zilizotolewa ni matumaini watawafikia wafugaji kwenye maeneo yao  kutoa elimu  kwani  kuna majosho 39  ambayo wanatakiwa kuyatumia ili kuwaondoa wadudu kupe ambao  wamekuwa wakishambulia  ngo’mbe.

 

Post a Comment

0 Comments