Header Ads Widget

KAMATI YA SIASA WARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA HOSPITALI MAGONJWA YA MLIPUKO-SHINYANGA

 Picha  ya  jengo la hospitali ya magonjwa ya mlipuko lililojengwa  eneo la Negezi kata ya Mwawaza manispaa ya Shinyanga.

 

Wajumbe wa Kamati ya siasi mkoa wa Shinyanga wakiwa picha ya pamoja baada ya ukaguzi wa ujenzi wa hosptali ya magonjwa ya mlipuko.


Wajumbe Wa Kamati Ya Siasa CCM Mkoa Wa Shinyanga wakitembelea kuona vyumba Vya madarasa na ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Lubaga.






Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,Mkoa wa Shinyaga Bw,Gasper Kileo  akifatilia maendeleo ya wanafunzi shule ya msingi Lubaga.

Na  Kareny  Masasy

WAJUMBE wa kamati ya siasa ya  chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Shinyanga wmekagua ujenzi  wa  hospitali ya magonjwa ya mlipuko  inayojengwa   eneo la Negezi kata ya Mwawaza manispaa ya  Shinyanga   nakurizishwa na kasi ya ujenzi huo.

 Kamati hiyo ikiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho mkoa   Mabala Mlolwa   jana  walikagua miradi mbalimbali iliyopo manispaa ya Shinyanga ikiwemo  ujenzi wa hospitali hiyo iliyogharimu kiasi cha zaidi ya sh Billioni moja na kukamilisha jengo.

Mlolwa amesema  kuwa  mradi huo umewafurahisha  kwa kujengwa kwa kiwango majengo yake na kuwataka viongozi wa mkoa kuutangaza ili wananchi waweze kuelewa vizuri   kweli Rais  Samia Suluhu amefanya kazi kubwa anastahili kupongezwa.

Kumekuwa na maneno kwa baadhi ya watu kuwa hatujafanya kitu leo nimejionea na kamati yangu majengo kama haya kwa mkoa wetu tulikuwa tunayaona mikoa mingine  hospitali hii itasaidia  kokoa maisha ya watu wengi ambao walikuwa wakipatwa na magonjwa walikuwa wakikimbilia mkoani Mwanza au Dar-es-salaam kutibiwa.” Alisema Mlolwa.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jansita Mboneko katika ziara hiyo  amesema  kuwa   mtu alivyokuwa akipatwa na magonjwa ya mlipuko mfano maambukizi ya Covid -19   ilikuwa ni changamoto  kubwa alilazimika kuwekewa mitungi minane hadi kumi ya kupumulia ili kuokoa maisha lakini sasa matibabu yatapatikana hapahapa  wilayani.

Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga Dkt  Augostino Maufi   akisoma taarifa mbele ya kamati hiyo ameeleza kuwa  ujenzi huo  mkataba wake ulianza rasmi mwaka jana mwezi Agosti nakutakiwa kukamilika  kipindi cha miezi sita na kiasi  cha zaidi  ya sh Billioni moja fedha kutoka kwa wafadhili wa Global  Fund na  serikali  zikitumika.

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments