Waziri wa Madini, Dkt.Doto Biteko Desemba  akizungumza na wachimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo la machimbo la
 Nyamalimbe Makarashani lililopo Wilaya ya Geita mkoani Geita. 
Wachimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo la machimbo la Nyamalimbe Makarashani lililopo Wilaya ya Geita mkoani Geita.
 Waziri wa Madini,Dkt.Doto Biteko akipokea maelezo  ya hali ya usalama wa wachimbaji dhahabu katika eneo la machimbo la
 Nyamalimbe Makarashani yaliyopo Wilaya ya Geita mkoani Geita.  
 Na mwandishi wetu.
WACHIMBAJI wa madini wametakiwa kuzingatia uchimbaji salama katika 
maeneo ya migodi yao ili waweze kufanya shughuli za uchimbaji madini kwa
 tija na migodi iendelee kubaki salama.
Hayo yameelezwa na Waziri
 wa Madini, Dkt.Doto Biteko lDesemba 29, 2021 alipokutana na kuzungumza 
na wachimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo la machimbo la Nyamalimbe
 Makarashani lililopo Wilaya ya Geita mkoani Geita.
Aidha, 
Dkt.Biteko amewaagiza wakaguzi wa mgodi katika machimbo hayo kuhakikisha
 wanaweka utaratibu wa daftari kwa ajili ya kuhifadhi kumbukumbu kwa 
kusainisha majina ya wachimbaji wanaoingia na kutoka katika machimbo 
hayo.
“Wasimamizi wote mnaosimamia hapa, hakikisheni watu 
wanaoingia kwenye duara kabla hajaingia kwenye duara kuna daftari juu, 
limeandikwa anatoka wapi na umri wake, anapozama na kutoka anasaini 
tena,”amesema Dkt.Biteko.
Kuhusu umuhimu wa kulipa kodi, 
Dkt.Biteko amesisitiza kila gramu ya dhahabu inayopatikana ipelekwe 
kwenye masoko ya madini ili Serikali ikusanye kodi. 
Aidha, 
amemuagiza Afisa Madini Mkazi wa Geita, Daniel Mapunda kutafuta wanunuzi
 wa madini ya dhahabu (Brokers) ili wasaidie kupunguza changamoto za 
wachimbaji kwenda umbali mrefu hadi Katoro kwa ajili ya kwenda kuuza 
dhahabu zao.
Kuhusu changamoto walizonazo hususani ya nishati ya 
umeme katika eneo hilo la machimbo, Dkt.Biteko amewahakikishia kwamba 
suala hilo limefanyiwa kazi kwa ushirikiano na Wizara ya Nishati ambao 
watafika kwa ajili ya kuwapatia umeme.
Aidha, Dkt.Biteko ameagiza
 mialo yote iliyopo katika maeneo ya maduara ya shughuli za uchimbaji 
madini yaondolewe ili zihamishiwe kwenye maeneo rasmi yaliyotengwa kwa 
ajili ya kuweka mialo hiyo.
Akizungumzia kuhusu kulinda afya za 
wachimbaji, Dkt.Biteko amesisitiza wachimbaji wa Nyamalimbe kuhakikisha 
wanalinda afya zao kutokana  na maradhi mbalimbali. 
Amesema, 
sehemu zenye shughuli za uchimbaji wa madini zina neema, lakini pia zina
 changamoto endapo mchimbaji hatazingatia taratibu za afya.
Naye,
 Jumanne Amani akisoma risala kwa niaba ya wachimbaji wa Nyamalinde 
amesema, uwepo wa mgodi katika  eneo hilo umeboresha maisha ya wakazi 
katika maeneo yanayozunguka mgodi huo na maeneo mengine ya watu 
wanaofika kujipatia kipato pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara.
Ameongeza
 kuwa, wachimbaji wa mgodi wa mlipuko wa dhahabu wa Nyamalimbe wanaomba 
kupatiwa huduma ya umeme katika eneo la mgodi ili kupunguza gharama za 
uendeshaji kwa wachimbaji na kuongeza tija.
 
 
       
 
 
