Header Ads Widget

PROF MANYA ATEULIWA KUJAZA NAFASI YA NAIBU WAZIRI ALIYESHINDWA KUAPA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Shukrani Manya kuwa Mbunge na Naibu Waziri wa Madini na ataapishwa leo mchana Ikulu Chamwino Dodoma.

Disemba 9,2020 Rais Magufuli alisema atafanya uteuzi wa Naibu Waziri mwingine wa Madini baada ya aliyemteua, Francis Ndulane Kumba ambaye ni Mbunge wa Kilwa Kaskazini kushindwa kuapa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma. 

Ndulane ambaye ni mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM) mwenye elimu ya shahada ya uzamili alikuwa mmoja wa waliotakiwa kuapa lakini alishindwa kusoma kiapo mbele ya Rais Magufuli, akikosea mara kadhaa kila alipopewa nafasi ya kurudia kusoma na ndipo katibu mkuu kiongozi, John Kijazi kumtaka aende kuketi kwanza ili wenzake waendelee kuapa.

Ndulane alisitasita na kukosea, kurudia hadi alipokatizwa na kutakiwa kupumzika.
CHANZO: Malunde 1 Blog

Post a Comment

0 Comments