Header Ads Widget

JESHI LA POLISI SHINYANGA LAKUTANA NA WADAU WANAOPINGA UKATILI WA KIJINSIA

 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza kwenye kikao kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili  wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo Jumanne Desemba 15,2020.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limeendesha Kikao Kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Kikao hicho kilichoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa Ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na Timu yake kimefanyika leo Jumanne Desemba 15,2020 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ukihudhuriwa na Maafisa wa polisi, Mahakimu, Maafisa Watendaji wa kata, Maendeleo ya Jamii, Asasi za kiraia, Mashirika, waandishi wa habari na wadau mbalimbali wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto. 

Katika kikao hicho wadau wamejadili kuhusu hali ya uhalifu kwa makosa ya ukatili wa kijinsia na watoto,upelelezi na changamoto za makosa ya kijinsia na watoto,kuendesha kesi za jinsia na watoto mahakamani,rushwa ya ngono na mpango Mkakati wa Mkoa wa Shinyanga katika kutokomeza Ukatili kwa wanawake na watoto mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 na Mpango Mkakati wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini wa mwaka 2017/18 – 2012/2025. 

Akifungua Kikao hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema suala la Ukatili wa Kijinsia na watoto ni mtambuka ambapo kila mtu ana wajibu wa kushiriki katika kutokomeza vitendo vya ukatili katika jamii. 

Alisema Ukatili wa kijinsia ni tatizo ambalo linapingwa kitaifa lakini bado linazidi kushamiri siku hadi siku kutokana na elimu duni kwa jamii pamoja na tamaduni, mila na desturi kwa jamii yetu. 

“Hatuna ubishi kuwa Shinyanga ni mkoa wenye jamii ya Kisukuma,kabila lenye imani zao kimila na siyo kazi rahisi kubadilisha mtazamo wa wenyeji kwa kipindi cha mwaka mmoja, miwili au mitatu bali muda wa kutosha unahitajika na inabidi tusichoke katika vita hii”, aliongeza Kamanda Magiligimba. 

Hata hivyo alisema Jeshi la polisi kupitia kitengo chake cha Dawati la Jinsia na Watoto linapambana katika kukamata,kuhoji mashahidi pamoja na kuandaa majalada kwa ajili ya kwenda mahakamani. 

“Na ifahamike kuwa kazi ya kuendesha mashtaka mahakamani ni ya Idara nyingine hivyo tunafanya kazi kwa kushirikiana ili kuleta ufanisi katika mashauri”,alifafanua. 

Aidha alisema bado kuna changamoto kubwa kama vile mtuhumiwa kukimbia baada ya kujua kuwa anatafutwa na polisi kwa kosa la kubaka,kumpa mimba mwanafunzi,kulawiti au mhanga kukaa na mtuhumiwa na wazazi au walezi kujadili namna ya kuwalipa wazazi wake fidia ili wasiendelee na shauri la ukatili mahakamani. 

Alitoa mfano mwingine kuwa ni pamoja na binti aliyetendewa ukatili kutoa ushahidi wa unaokinzana na na maelezo yake akiwa anahojiwa kituo cha polisi huku akijaribu kumficha mtuhumiwa aliyetenda kosa hilo. 

“Hizi sababu zinasababisha kesi kukosa ushahidi wa kutosha kumtia hatiani mtuhumiwa hivyo kuachiwa huru na inawezekana akifika mtaani ataendelea na vitendo hivyo kwani hakuweza kupata adhabu sahihi dhidi yake",alisema Kamanda Magiligimba. 

"Kutokana na kauli mbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia inayosema “Tupinge Ukatili wa Kijinsia Mabadiliko yanaanza na Mimi” yatupasa sote kutimiza wajibu wetu katika kuwalinda watoto wa kike na kiume kwani ndiyo taifa letu la kesho”,aliongeza. 

Katika hatua nyingine alitoa wito kwa maafisa watendaji wa kata na vijiji waache kushiriki kumaliza kesi za ukatili wa kijinsia kifamilia. 

Naye Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Shinyanga SP Davis Msangi aliyataja matukio ya ukatili wa kijinsia na watoto yanayoripotiwa zaidi Polisi kuwa ni ubakaji, mimba za utotoni,ulawiti, kushindwa kuhudumia familia, kutupa watoto na shambulio la aibu.

Mkuu huyo wa Upelelezi alishauri siku ya kusomwa kesi mtu aliyefanyiwa ukatili wa kijinsia anatakiwa kuwepo mahakamani ili kutoka ushahidi huku akiviomba vyombo vya habari kutangaza matokeo ya kesi za ukatili wa kijinsia na watoto hasa adhabu zinazotolewa kwa wahusika wa matukio ya ukatili ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto , Tedson Ngwale alisisitiza Maafisa Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Watendaji wa kata kusimama vema katika nafasi zao ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi na usalama wa Watoto ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya ndoa kabla ya kufungwa ili kubaini umri wa wanandoa na hali za shule na kufanya ufuatiliaji wa Watoto wote wanaohamishwa shule ili kujua kama kweli shule walizohamishiwa wameripoti.

Akitoa mada kuhusu changamoto katika kuendesha kesi za jinsia na watoto mahakamani na ushauri ili kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia na watoto Wakili wa Serikali Mwandamizi Salome Mbuguni  kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga aliwataka wazazi na walezi.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Shinyanga, Mary Peter Mrio akizungumza kwenye kikao cha wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto aliomba wadau wote kushirikiana kwa pamoja ili kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Kwa upande wao washiriki wa kikao hicho walisema umaskini na utoro wa wanafunzi shuleni umekuwa ukichangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto huku wakibainisha kuwa kesi za matukio ya ukatili wa kijinsia na Waathirika wa matukio ya ukatili kuchelewa kupata huduma inasababisha washindwe kupata huduma kwa wakati.

Aidha wameshauri  elimu itolewe kwa jamii kuhusu madhara ya ukatili wa kijinsia na umuhimu wa kutoa ushahidi mahakamani wakisisitiza pia umuhimu wa  suala la ukatili wa kijinsia liwe ajenda kwenye mikutano na vikao vyote vya maamuzi kuanzia ngazi ya kijiji na kata. 

Wadau hao pia wamewataka baadhi ya watu wenye mamlaka na madaraka mfano hospitalini, polisi, mahakamani kuacha kuendekeza rushwa kuzima matukio ya ukatili wa kijinsia kwani rushwa inafifisha haki za waathirika wa matukio ya ukatili wa kijinsia na watoto.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo Jumanne Desemba 15,2020 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Kikao hicho kimeandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwa Ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto .Kushoto ni Mkuu wa Operasheni wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Jackson Martin Mwakagonda. 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto .Kushoto ni Mkuu wa Operasheni wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Jackson Martin Mwakagonda.
Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Shinyanga SP Davis Msangi akitoa mada kuhusu hali ya uhalifu kwa makosa ya ukatili wa kijinsia na watoto,upelelezi na changamoto za makosa ya jinsia na watoto.
Wakili wa Serikali Mwandamizi Salome Mbuguni kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga akitoa mada kuhusu changamoto katika kuendesha kesi za jinsia na watoto mahakamani na ushauri ili kutokomeza matukio ya ukatili wa kijinsia na watoto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akifuatilia uwasilishaji wa mada kwenye kikao kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Shinyanga, Mary Peter Mrio akizungumza kwenye kikao cha wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto.

Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto , Tedson Ngwale ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Shinyanga, akiwasilisha mada kuhusu Mpango Mkakati wa Mkoa wa Shinyanga katika kutokomeza Ukatili kwa wanawake na watoto mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 na Mpango Mkakati wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini wa mwaka 2017/18 – 2012/2025.
Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Shinyanga Winfredy Komba akiwasilisha mada kuhusu Rushwa ya ngono na mtazamo wa kisheria katika kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Hakimu Mkazi Shinyanga Mahakama ya Hakimu Mkazi Shinyanga, Proches Mushi akizungumza kwenye kikao kazi na wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Kikao kinaendelea
Mkuu wa Operasheni wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Jackson Martin Mwakagonda akizungumza kwenye kikao cha wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto.
Kikao kinaendelea
Kikao kikiendelea
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wakiwa ukumbini
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Kikao kinaendelea

Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakiwa ukumbini.
Kikao kinaendelea
Mkaguzi wa Msaidizi wa Polisi Analyse Desdery Kaika kutoka Ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga akisisitiza jambo kwenye kikao kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakifanya majadiliano kwenye vikundi namna ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakifanya majadiliano kwenye vikundi namna ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakifanya majadiliano kwenye vikundi namna ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakifanya majadiliano kwenye vikundi namna ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Wadau wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto wakifanya majadiliano kwenye vikundi namna ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na watoto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba (kulia) na Mkuu wa Operasheni wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Jackson Martin Mwakagonda wakiwa kwenye kikao cha wadau kujadili masuala ya ukatili wa kijinsia na watoto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akifunga kikao kazi na Wadau Wanaopinga Ukatili wa Kijinsia na Watoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kujadili mkakati wa mkoa wa Shinyanga katika kupambana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto leo Jumanne Desemba 15,2020 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. 


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Post a Comment

0 Comments