Header Ads Widget

TVMC LAFANYA BONANZA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO DIDIA

Wanafunzi wakisikiliza nasaha wakati wa ufunguzi wa Bonanza hilo la michezo la kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Na Marco Maduhu- Shinyanga
Shirika la TVMC linalotetea haki za Wanawake na Watoto mkoani Shinyanga limefanya Bonanza la michezo kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari Kata ya Didia Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Bonanza hilo limefanyika leo kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari DonBosco na kuhudhuliwa na wanafunzi, walimu, watendaji wa Kata, vijiji, Maofisa Ustawi wa jamii, Maendeleo, pamoja na dawati la jinsia kutoka Jeshi la Polisi, kwa ufadhili wa Shirika la Foundation for Civil Society.

Shule zilizohudhuria Bonanza hilo ni Shule ya Msingi Didia, Bugisi, Mwamalulu, Mwanono, Bukumbi, pamoja na Ola, huku Shule za Sekondari ni Didia na DonBosco.

Akizungumza kwenye bonanza hilo, Mkurugenzi wa Shirika la TVMC, Mussa Ngangala amesema tukio hilo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wao wa kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto kwenye Kata hiyo ya Didia.

Amesema moja ya njia ya kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, ni kuendesha mabonanza ya michezo ambayo hukusanya wanafunzi wengi kwa wakati moja.

"Dhumuni la kufanya Bonanza hili la michezo ni kufikisha ujumbe wa kupinga vitendo vya ukatili ndani ya jamii, dhidi ya wanawake na watoto, ili kuifanya jamii iwe salama," amesema Ngangala.

"Vitendo vya ukatili ambavyo tunavipinga, ni vipigo kwa wanawake, na watoto, utumikishaji watoto, kuwanyima haki ya kupata elimu, pamoja na tatizo la mimba na ndoa za utotoni," ameongeza.

Pia Ngangala amewataka wanafunzi kupaza sauti pale wanapofanyiwa vitendo vya ukatili, na siyo kukaa kimya, ili wahusika wachukuliwe hatua kali, jambo ambalo litatokomeza matukio hayo.

Naye mgeni Rasmi kwenye Bonanza hilo, Afisa Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Beda Kamala akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Jasinta Mboneko, amewataka wanafunzi hasa wa kike, wasome kwa bidii ili watimize ndoto zao ,pamoja na kukataa kufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia. 

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Afisa Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Beda Kamala akizungumza kwenye bonanza hilo.
Afisa Maendeleo wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Opeyo Sisso akizungumza kwenye bonanza hilo na kuwataka wanafunzi wasome kwa bidii ili watimize ndoto zao.
Mkurugenzi wa Shirika la TVMC, Mussa Ngangala, akizungumza kwenye kongamano hilo na kuwataka wanafunzi wapaze sauti za ukatili wa kijinsia kwa kutoa taarifa ili wahusika wachukuliwe hatua.
Mkurugenzi wa Shirika la TVMC, Mussa Ngangala akielezea madhumuni ya Bonanza hilo la kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Wanafunzi wakisikiliza nasaha wakati wa ufunguzi wa Bonanza hilo la michezo la kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.
Afisa Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Beda Kamala akipiga mpira kuashiria kufungua bonanza hilo.
Wanafunzi wakishiriki bonanza hilo katika mchezo wa riadha.
Wanafunzi wakishiriki mchezo wa kukimbiza kuku, ambapo mshindi ameondoka na kuku huyo
Zoezi la ufukuzaji kuku likiendelea.
Wanafunzi wakishindana kukimbia katika magunia.
Wanafunzi wakishindana kukimbia katika magunia.
Wanafunzi wakicheza mpira wa Pete.
Wanafunzi wakicheza mpira wa wavu.
Mpira wa kikapu ukiendelea kuchezwa.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Didia (jezi nyeusi), pamoja na Wanafunzi wa shule ya Sekondari DonBosco (Jezi ya Orange), wakitoa Burudani kwenye Bonanza hilo la michezo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Didia,( Jezi Nyekundu) na Mwanono (Jezi Nyeupe na mistari nyeusi) wakitoa burudani kwenye bonanza hilo.
Burudani ya mpira wa miguu ikiendelea kutolewa.
Penalti zikipigwa mara baada ya Timu za DonBosco na Didia Sekondari kutoka bila ya kufungana.
Penalti zikipigwa mara baada ya Timu za DonBosco na Didia Sekondari kutoka bila ya kufungana, ambapo katika Penalti hizo, Timu ya Didia Sekondari waliibuka na Ushindi.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Wanafunzi wakiwa kwenye Bonanza wakitazama michezo mbalimbali ikichezwa.
Afisa Tawala wa Wilaya ya Shinyanga, Beda Kamala (kulia), akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi katika bonanza hilo la michezo.
Beda Kamala akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi

Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Beda Kamala, akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi katika Bonanza hilo la Michezo.
Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Beda Kamala, akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi katika Bonanza hilo la Michezo.
Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Beda Kamala, akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi katika Bonanza hilo la Michezo.
Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Beda Kamala, akigawa zawadi mbalimbali kwa washindi katika Bonanza hilo la Michezo lililoandaliwa na Shirika la TVMC kwa ufadhili wa Shirika la Foundation for Civil Society.