
Na Suzy Luhende
Shinyanga
Kikao cha Baraza la Madiwani
wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga kimeazimia kuwafukuza Kazi
watumishi wanne wa halmashauri hiyo
baada ya kubainika kuhusika na upotevu wa fedha Sh milioni 20 na makosa ya nidhamu na utoro kazini .
Akizungumzia maamuzi hayo yaliyoazimiwa Mei 19 mwaka huu, Mwenyekiti
wa halmashauri ya Kishapu, Boniface Butondo amesema watumishi hao wamekosa
nidhamu ya utumishi wa umma wakiwa kazini baada ya kuonekana kuhusika na
upotevu wa fedha za Serikali licha ya kutakiwa kuzirejesha.
Amewataja watumishi hao kuwa ni Ally
Mussa aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha
Pumbula Kata ya Songwa,Njile
Kwilasa aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Mihama Kata ya Lagana,Marimu Manyirizu kutoka
idara ya mifugo ambaye amekuwa mtoro kazini kwa muda mrefu zaidi ya siku 100 na hajulikani alipo.
Mwingine ni Nkonya Charles aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Talaga
wilayani humo,ambapo Butondo amewataka watumishi wote wafanye kazi kwa bidii na uaminifu.
“Halmashauri tutaendelea na utaratibu wa kuwafukuza na kuwasimamisha kazi watumishi wote wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi zao,ili kuhakikisha kuna kuwa na nidhamu na kuzuia upotevu wa fedha za serikali''alisema Butondo.
Aidha Mwenyekiti huyo amefafanua kuwa kabla ya maamuzi hayo watumishi hao waliitwa na kutakiwa kurejesha fedha kwa wakati na tayari wamefikishwa kwenye kamati lakini hawajarudisha na kulilazimu baraza kufikia maamuzi hayo.
Baadhi ya madiwani akiwemo Frednand Mpogomi na Felister Nkinga wamepongeza maamuzi hayo kwani watumishi hao walipewa nafasi ya kurudisha fedha hizo lakini hawakutekeleza hadi leo.
Tazama picha mbalimbali za kikao hicho








Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464