Header Ads Widget

SIMBA SC KUANZA MAZOEZI JUMATANO, WACHEZAJI KUWASILI JUMATATU





Baadhi ya viongozi wa Klabu ya Simba wakizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam




Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Senzo Mbatha akisisitiza jambo  wakati wa mkutano na waaandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.



Na Damian Masyenene na Mitandao

ILE hamu ya mashabiki na wadau wa soka nchini iliyokuwa inasubira kufahamu nini kitajiri leo saa 7 mchana kutoka klabu ya Simba, hatimaye  imejibiwa ambapo Wekundu hao wa Msimbazi wametangaza kuanza kujifua rasmi Jumatano Mei 27, mwaka huu.


Simba SC wametangaza uamuzi huo kupitia kwa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Senzo Mbatha leo saa 7 mchana katika mkutano wao na wanahabari jijini Dar es Salaam baada ya kuweka kibwagizo kwa takribani siku tatu kikiwaacha njia panda mashabiki ambao walisubiria kufahamu ni nini kitajiri.

"Tumeanza mipango yetu na tumepanga kuanza mazoezi Jumatano baada ya Eid."- CEO Senzo Mbatha
Mbatha raia wa Afrika Kusini ameweka wazi kuwa wachezaji wote wa tmu hiyo waliopo nje ya nchi tayari wamefanya mawasiliano nao na wataanza kuwasili kabla mazoezi hayajaanza siku ya Jumatano.

"Wachezaji wetu wote ambao wapo nje ya Tanzania tunawasiliana nao na mmoja kati ya wachezaji hao atakuwepo nchini Jumatatu. Wengine tunatarajia watakuwepo nchini kabla hatujaanza mazoezi."- CEO Senzo Mbatha.

"Lazima tujikite kuhakikisha tunashinda ligi kuu na FA. Hiyo ndio dhamira wetu kwa sasa."- CEO Senzo Mbatha.

Katika hatua nyingine Klabu hiyo ya mitaa ya Msimbazi imezindua rasmi tovuti yake ambayo itakuwa na habari, matukio na Ratiba, timu, historia ya klabu, matukio yote ya klabu, sehemu ya mashabiki, huku wakiweka wazi kuwa watazindua App ya klabu hiyo wiki ijayo.

Wekundu wa Msimbazi Simba SC ambao ni mabingwa watetezi wa Lgi Kuu Tanzania bara wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi 17 wakiwa kileleni na alama 71 wakifuatiwa na Azam FC yenye pointi 54 na Yanga yenye alama 51, ambao kutangaza kuanza mazoezi kwa tmu hiyo ni mwitikio wa tamko la Serikali kuruhusu michezo kurejea ifikapo Juni Mosi, mwaka huu.