
Baadhi ya wakazi na wavuvi wa kisiwa cha Muchangani Kata ya Kome halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema wakiangalia jinsi moto uivyoathiri mali zao.

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Maria Bundala (40) amefariki
dunia huku magari matano na vibanda zaidi ya 150 kuwaka moto baada ya moto
kuzuka katika kambi ya wavuvi ya Kisiwa cha Kome kilichopo wilayani Sengerema
Halmashauri ya Buchosa.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Muliro Jumanne Muliro, amesema eneo hilo
lina Mkusanyiko wa watu zaidi ya elfu 3,000 huku Shughuli kubwa ikiwa ni
uvuvi. "Majira ya saa 6:1 usiku kulitokea tukio hilo ambapo
baada ya kufika eneo hili tumebaini mtu mmoja anayejulikana kwa jina la
Maria Bundala (40) amepoteza maisha huku magari zaidi ya manne aina ya fuso na
vibanda vilivyojengwa katika mfumo wa kufanya kazi mbalimbali na makazi
vikiteketea kwa moto,." amesema Kamanda Murilo
Kamanda
Murilo amesema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama
wanafanya tathimini ili kujua ni kwa kiwango gani cha athari kimetokea huku usalama ukiimarishwa katika eneo hilo.
Noel
Sangija ni mmoja wa wakazi waliokubwa na adha hiyo amesema janga hilo limesababishwa
na mamalishe kusahau kuzima moto baada ya kupika chakula kwani moto ulipo anzia
ndipo mafiga yalipo , hivyo waliiomba serikali kuwatengenezea mpango mkakati wa
unjezi mzuri ili kujinusuru na majanga kama hayo.
“Tumeuguza
samaki zenye gharama kubwa hii ni mara ya tatu majanga kama haya
yananikuta ambapo mara ya kwanza aliunguza gesti mbili ,mara ya pili na kipindi
hiki ameunguza gesti yenye vumba 24 ,mwanzoni tulikuwa na utaratibu wa
kuzunguka kwa wale wanaopika karibu na makazi ya watu”anasema Sangija.
Akizungumza
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mangella, Mkuu wa Wilaya ya
Sengerema, Emmanueli Kipole ametembelea eneo hilo akiwa na kamati ya ulinzi na
usalama mkoa kwa lengo la kuhakikisha usalama unaimarishwa katika eneo hilo.
Kama
ilivyo katika matukio kama haya kuna baadhi ya watu wasio na utu wanaona hii ni
fursa kwao hivyo natoa onyo kwa watu mwenye tabia hizo waache na vitu
vilivyookolewa vibaki salama sihitaji kuona mtu anafanya mambo ya hovyo
kamati ya usalama mkoa na wilaya itakuwepo hapa hadi mambo yawe shwali”
amesema Kapole
Amewataka
wakazi wa eneo hilo kurejea katika vijiji vyao ili mahali hapo
palekebishwe lakini watambue Serikali inatambua michango yao katika
kujenga taifa na itakuwa pamoja nao.
Chanzo IPP MEDIA/Nipashe.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464