
Na
Mwandishi wetu
Imeelezwa kwamba msimamo wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli kuamua kupita njia ya
kipekee na kuwa na maamuzi tofauti na mataifa mengine yote duniani katika
kutafuta ufumbuzi wa Mapambano ya virusi
vya Corona ikiwemo kukataa kupitisha uamuzi wa kuwafungia watu ndani ‘Lockdown’
umelisaidia taifa kupiga hatua kubwa katika mapambano hayo ya ugonjwa wa
COVID-19.
Hayo yameelezwa na Askofu wa
Kanisa la International Evangelical Assemblies of God Tanzania (IEAGT) la mjini
Shinyanga, Askofu David Mabushi leo Mei 24, 2020 katika ibada ya Jumapili Kanisani
hapo ambapo ameipongeza Serikali kwa njia walizotumia kupunguza maambukizi ya COVID-19 kwa kuwa tofauti sana na dunia nzima kupitia
ushauri wa shirika la afya dunia WHO
.
Mabushi amesema kuwa kutowafungia
watanzania majumbani (lockdown) na kuwaondolea wananchi hofu kwa kubana taarifa
za hali ya maambukizi imesaidia kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya
mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona.
“Tuliona mitazamo ya wanasayansi
wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na wanasiasa wengi wa dunia wakilazimisha watu
wafungiwe ndani lakini njia hizo zimesababisha dunia nzima kupata shida tofauti
na taifa letu lililochagua mbinu nyingine.
“Nampongeza sana Rais wetu kwa
njia alizotumia kupambana na janga hili, tunaona kwa sasa hata mataifa mengi ya
dunia yameanza kufungua mipaka yao na wengine kuruhusu shughuli za ibada
kuendelea kama kawaida,” amesema Askofu Mabushi.
Askofu Mabushi ameongeza kwa
kusema kuwa kukaa Majumbani bila shughuli yoyote kuna changia kupunguza kinga
za mwili, huku utoaji wa taarifa nyingi zenye kujenga hofu kwa wananchi kuna sababisha
wananchi kufariki kwa hofu.
Kwa upande wao baadhi ya
waumini wa Kanisa hilo akiwemo Leonard
Kajiba na Neema Elias wameupongeza uamuzi wa Rais wa Kutoifungia nchi kwani
kungesababisha jamii kubwa ya watanzanai kuteseka kutokana na wengi wao hutegemea
kutoka nje kufanya shughuli mbalimbali na kujipatia kipato kwa ajili ya maisha
yao ya kila siku.
Ibada hiyo ni sehemu ya siku tatu zilizotengwa kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kuliepusha taifa na Maambukizi makubwa ya Corona kutokana na idadi ndogo ya maambukzi ya Covid- 19.
Ibada hiyo ambayo imetumika kwa waumini wa kanisa hilo
kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kulisaidia taifa la Tanzania kuvuka salama katika
kipindi hiki kigumu baada ya kusali na kuomba kwa miezi kadhaa, ambapo pia
Serikali ilitenga siku tatu kwa wananchi kumshukuru Mungu.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464