Header Ads Widget

Picha : WAANDISHI WA HABARI SHINYANGA WAPATIWA VIFAA VYA KUJIKINGA NA CORONA



Na Damian Masyenene - Shinyanga Press Club

Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga(SPC) imegawa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya virusi vya homa kali ya mapafu Corona kwa waandishi wa habari,ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao katika mazingira salama na kuepuka maambukizi.

Vifaa walivyopewa wanachama ni barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni za maji ‘Hand soaps’ ambapo zoezi la ugawaji vifaa hivyo limesimamiwa na Viongozi wa SPC wakiongozwa na Mwenyekiti wa SPC Kadama Malunde kwa waandishi wa habari waliopo Shinyanga Mjini na Makamu Mwenyekiti wa SPC, Shaban Alley kwa waandishi wa habari waliopo Kahama Mjini.

Akigawa vifaa hivyo leo Mei 29 kwa wanachama wa SPC ,Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Kadama Malunde amesema kuwa,vifaa hivyo vimetolewa na Muungano wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania kwa wanachama wake kuwakinga na virusi vya Corona.

Malunde amewataka waandishi wa habari kuendelea kuchukua tahadhari na kufuata masharti na miongozo inayotolewa na Wizara ya Afya.

Malunde amesema kila mwandishi ambaye ni mwanachama wa SPC amepata barakoa nne, sabuni ya kunawia moja, vitakasa mikono viwili na gloves tatu,huku akiwaomba wadau wengine kusaidia waandishi wa habari vifaa vya kujikinga na Corona kwa kuwa ni kundi ambalo linakutana na watu wengi.

“UTPC iliona ni vyema kuwapatia vifaa waandishi wa habari kwani ni kundi ambalo linakutana na watu mbalimbali na huwezi kujua ni nani ana virusi vya Corona,ndiyo maana tumegawa vifaa hivyo viweze kuwasaidia wanapokuwa kazini”,amesema Malunde.

Nao baadhi ya waandishi wa habari wameishukuru UTPC kwa kutoa vifaa hivyo kwa waandishi wa habari kupitia kwenye Klabu za waandishi wa habari kwani vitakuwa ni msaada mkubwa katika kazi zao katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya Corona.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni za maji ‘Hand soaps’ kwa ajili ya waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 29,2020. Kushoto ni Mweka Hazina wa Shinyanga Press Club, Stella Ibengwe. Picha na Shinyanga Press Club
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kujikinga na Corona kwa waandishi wa habari ambapo amewasisitiza kuendelea kuchukua tahadhari kuhusu Ugonjwa huo.
Muonekano wa vifaa vya kujikinga na Corona vilivyotolewa kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Awali Mratibu wa Shinyanga Press Club, Estomine Henry (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde kabla ya kuanza kugawa vifaa hivyo kwa wanachama wa SPC
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club -SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mweka Hazina wa Shinyanga Press Club, Stella Ibengwe ambaye ni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Mwananchi.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Radio Faraja, Moshi Ndugulile.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Radio Faraja, McDonald Masse.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Radio Kwizera, Amos John.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Mtanzania, Damian Masyenene.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Habarileo, Kareny Masasy.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Radio Faraja, Stephen Kanyefu.
Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Radio Free Africa, Shangwe Than.
Mwandishi wa habari wa Radio Free Africa, Shangwe Than akizungumza jambo wakati akipokea vifaa vya kujikinga na COVID - 19.
Kushoto ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Majira Suleiman Abeid.
Kushoto ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe, Marco Maduhu.
Kushoto ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) , Kadama Malunde akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Mtanzania, Sam Bahari.
Sehemu ya wanachama wa Shinyanga Press Club Mjini Shinyanga wakiwa na vifaa vya kujikinga na COVID -19.
Sehemu ya wanachama wa Shinyanga Press Club Mjini Shinyanga wakiwa na vifaa vya kujikinga na COVID -19.
KAHAMA: Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) Shaban Alley akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Katibu wa Shinyanga Press Club, Ally Lityawi ambaye ni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima.
Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) Shaban Alley akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Katibu wa Shinyanga Press Club, Mwandishi wa habari wa Gazeti la Majira, Patrick Mabula.
Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) Shaban Alley akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Katibu wa Shinyanga Press Club, Mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru, Salvatory Ntandu.
Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) Shaban Alley akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe, Neema Sawaka.
Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club - SPC) Shaban Alley akimkabidhi vifaa vya kujikinga na COVID -19 ikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni Mwandishi wa habari wa Gazeti la Nipashe, Shaban Njia.
Wa Kwanza kushoto ni Mwandishi wa Radio Huheso Fm, Chevawe Mandari,akifuatiwa na Neema Sawaka wa Gazeti la Nipashe,Othman Nyamiti wa Divine Fm, Shaban Alley wa Star Tv, Ally Lityawi wa Gazeti la Tanzania Daima na Paul Kayanda wakiangalia vifaa kwa ajili ya kujikinga na COVID -19 zikiwemo barakoa (masks), vitakasa mikono (sanitizers), medical gloves na sabuni. 
Sehemu ya Wanachama wa Shinyanga Press Club waliopo Kahama Mjini wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya kupokea vifaa kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya COVID -19.
Sehemu ya Wanachama wa Shinyanga Press Club waliopo Kahama Mjini wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya kupokea vifaa kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya COVID -19.

Picha na Shinyanga Press Club