Mhe. Lazarus Chakwera, Rais wa Zamani wa Malawi, akiambatana na Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe. Shirley Ayorkor Botchwey, amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, jijini Dar es Salaam Aprili 9, 2026.
Mkutano huo ulilenga kumkaribisha nchini na pia ni ishara ya kuanza ratiba yake ya kukutana na wadau mbalimbali ikiwamo kukutana na ujumbe wa Serikali Aprili 09, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464












