` WAMACHINGA -KAHAMA WATAKA MIKOPO NA MAENEO MAALUM YA BIASHARA

WANDAMAN HOTEL

WAMACHINGA -KAHAMA WATAKA MIKOPO NA MAENEO MAALUM YA BIASHARA


 

Na Kareny  Masasy,

Kahama

KATIBU wa Nec,Siasa Uhusiano wa Kimataifa (SUKI) Rabia Hamad ,amesema kuna  mkakati  wa kuweka machinga Complex kwenye kila wilaya ili machinga wote wawe sehemu moja nakuweza kutambulika.

Hamad amesema  tarehe 26/03/2026  kwenye kikao kazi wilayani Kahama  kilichowakutanisha makundi ya wajasiliamali, Watu wenye Walemavu,Wachimbaji Wadogo na  Wawezeshaji wanawake kiuchumi huku akisisiiza kukopa kwenye Halmashauri na Benki ambako kuna fedha ziko huko.

Hamad alisema wajasiriamali waendelee kukaa kwenye vikundi nakupata mikopo isiyo na riba kwenye   Halmashauri na ile ambayo Rais Samia Suluhu  aliitoa kwenye benk ya NMB  kwa mashariti nafuu na lazima uwe na   kitambulisho cha mjasiliamali.

Viongozi mnapoona kimpya  muhoji kwanini hiki hakijatekelezwa au kimefikia wapi ili ngazi ya juu iweze kulifanyia kazi”amesema  Hamad.  

Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa  Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Makundi Maalum  Slyilivia Lusumo alisema wafanyabiashara wote wadogo wanatakiwa kutambulika kwa mauzo kwa mwaka yasizidi Milioni Nne huku wakitoa changamoto ya fursa za mikopo haziwafikii.

Serikali imetoa shilingi bilioni 200 na zimewekwa katika mgawanyo mpaka sasa zimetolewa bilioni 12 na nchi nzima na mkoa wa Shinyanga zimetolewa shilingi  Milioni 255 kwa wafanyabiashara 124”amesema  Lusumo.

 Lusumo alisema wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga waliosajiliwa ni  1556  na waliosajiliwa  ni wafanyabiashara ni 750 na utaratibu wa kupata mkopo nilazima uwe umesajiliwa kwenye mfumo na vigezo wawe na  utambulisha  wa  mjasiliamali.

Ofisa Maendeleo ya Jamii Khamis  Mnubi alisema  vigezo  vya kupata mkopo kikundi lazima kisajiliwe na mkazi wa eneo husika  nakuomba kupitia mkopo hivyo halmashauri inajitosheleza kwani  mwaka huu wa fedha 2025/2026  wametenga  billion 3  wametoa mikopo kwenye awamu mbili  kuanzia mwezi Julai hadi Disemba  shilingi bilioni 1.1 katika vikundi 57.

Akiongea kwa niaba ya Umoja wa machinga (Shiuma) wilaya ya Kahama  Barnaba Mazengo  amesema Kahama  inahudumia nchi nane lakini  hawana eneo maalum la machinga  (Machinga compelx) ambapo hakuna miundombinu mizuri.

 “Wapo wanufaika wa mikopo ambao wanamitaji tayari na wale ambao wanachuuza biashara zao mitaani hawana sifa sababu hawana kizimba nakukipata ni shilingi 50,000  nakulipa ni muda wa miezi sita na hela hawana”amesema  Mazengo.

Mwisho.





Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464