` CRDB YALETA TABASAMU IGUNGA: MADAWATI 40 YABADILISHA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA SHULE YA HANIHANI

CRDB YALETA TABASAMU IGUNGA: MADAWATI 40 YABADILISHA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA SHULE YA HANIHANI


Meneja wa CRDB Bank Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana akikabidhi msaada wa madawati 40 kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Igunga  Mkoa wa Tabora Elizabeth Rwegasira ambaye pia ni Katibu Tawala Wa wilaya hiyo,madawati  ambayo yametolewa  kwa shule ya msingi Hanihani  ili kusaidia upungufu wa madawati katika shule hiyo.
    
Meneja wa CRDB Bank Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana akizungumza na walimu,wazazi na wanafunzi katika shule ya msingi Hanihani baada ya kukabidhi msaada wa madawati.

                   Na Stella Herman, Tabora

Katika mwendeleo wa kuhakikisha wanasaidia kupunguza changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu,CRDB Bank imetoa msaada wa madawati 40 kwa shule ya msingi Hanihani Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora.

 

Akikabidhi madawati hay oleo Desemba 05,2025 Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wambura Wagana,amesema hatua hiyo inasaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati na kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri.

 

Amesema CRDB Bank inawajali wateja wake kwa kutoa misaada inayogusa Jamii ikiwa ni kurejesha sehemu ya faida yake kwa Jamii,kwa kuangalia changamoto zilizopo ili kusaidia kupeleka msaada.


“Tulipata maombi kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga kwamba kuna upungufu wa madawati kwa baadhi ya shule,na sisi kama wadau wa maendeleo tukaona tupeleeeke msaada hata kwa shule moja na tunafanya hivyo kupitia kampeni ya CRDB" keti jifunze" ambayo iko nchi nzima”amesema Wagana 

Amewataka wanafunzi kuyatunza madawati hayo ili yaweze kudumu na kusaidia wengine kama wao walivyokuta madawati yaliyopo ambayo yalitunzwa na waliowatangulia kuanza kusoma.

                              
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Hanihani

                                       

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Igunga Elizabeth Rwegasira ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Igunga, ameishukuru CRDB kwa msaada wa madawati kwani umesaidia kupunguza tatizo la wanafunzi kukaa chini ambapo wanafunzi 120 wanakaa chini.


Amesema CRDB Bank ni mdau mkubwa katika kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo katika sekta ya elimu,afya na mazingira,ambapo leo kupitia msaada wa madawati umesaidia kuwawezesha wanafunzi kuondokana na adha ya kusoma wakiwa wamekaa chini. 

                      
  Mwita Ally Meneja Mahusiano idara ya serikali Kanda ya Magharibi CRDB Bank
                                        
                                        

                                        

                 Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Igunga  Joseph Mafuru 

                                        
                                               

Michael Mahushi Katibu wa Mbunge Jimbo la Igunga
                                                                   

                                         


                                      





                       

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464