` RAHMA: KATAMBI KIONGOZI KIJANA, SHUPAVU,MNYENYEKEVU AMPIGIA DEBE AONGOZE MITANO TENA JIMBO LA SHINYANGA MJINI KUTOKANA NA KUPIGA KAZI KUBWA YA MAENDELEO

RAHMA: KATAMBI KIONGOZI KIJANA, SHUPAVU,MNYENYEKEVU AMPIGIA DEBE AONGOZE MITANO TENA JIMBO LA SHINYANGA MJINI KUTOKANA NA KUPIGA KAZI KUBWA YA MAENDELEO


Na Mwandishi Wetu.

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Patrobas Katambi, amepewa sifa kemkem akitajwa kuwa kiongozi kijana, shupavu, mnyenyekevu, na mwenye maono makubwa ya kuendeleza maendeleo.

Kutokana na mafanikio aliyoyapata katika awamu ya sita ya uongozi (2020–2025), Kada wa CCM, Rahma Kware, amesisitiza kuwa wananchi wa Shinyanga hawana sababu yoyote ya kubadilisha uongozi bali Katambi anatoshwa na apaswa kupigia kura nyingi za ushindi siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29.

Kutoka Milioni 800 hadi Bilioni 7: Kuongezeka kwa Makusanyo

Rahma amemsifia Katambi,kwamba ametekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa kugusa sekta zote,na kuleta heshima kubwa katika mji wa Shinyanga.

Rahma amesema, katika mikutano ya kampeni ya Katambi aliyohudhuria amefarijika kusikia  uimara wa uongozi wake kwa kuelezea namna alivyoongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato  Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, kwamba awali kilikuwa kikikusanywa kiasi cha fedha wastani wa Shilingi milioni 800 pekee kwa mwaka. Lakini kwa sasa, makusanyo yameongezeka kwa kasi kubwa na kufikia Shilingi bilioni 7.

Mafanikio Yaliyoainishwa Kisekta:

Ametaja pia Mafanikio ya Katambi katika jimbo la Shinyanga Mjini yameonekana katika sekta mbalimbali za kijamii na miundombinu.

Sekta ya Afya

Katika sekta ya afya, Katambi amesaidia:

  • Kufanikisha upatikanaji wa zaidi ya Shilingi bilioni 7.5 kwa ajili ya kukamilisha jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mwawaza, ambalo sasa limewezeshwa kwa vifaa tiba vya kisasa, pamoja na upatikanaji wa dawa.
  • Kusaidia kupatikana kwa ambulance nne.
  • Kufanikisha ujenzi wa zahanati nane katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.

Sekta ya Elimu

Mafanikio katika elimu ni pamoja na:

  • Kuhusishwa na ujenzi wa shule 11 (ambazo ni shule sita za msingi na tano za sekondari).
  • Kuanzishwa kwa taasisi za elimu ya juu zikiwemo Chuo Kikuu cha Ushirika Kizumbi, Chuo cha Madini, na Chuo cha Serikali za Mitaa.

Miundombinu (Umeme, Barabara, na Maji)

Katika kuboresha miundombinu, yafuatayo yamefanyika:

  • Umeme: Vijiji 55 vimeunganishwa na huduma ya umeme.
  • Barabara: Barabara nyingi zilizokuwa hazipitiki sasa zimewekewa madaraja ya kisasa.
  • Maji: Sekta hii imepata mabadiliko makubwa kupitia mtandao mpya wa maji unaojulikana kama “DP System”, wenye mifumo miwili ya maji safi na maji taka. Mfumo huu umesababisha gharama ya maji kushuka hadi Shilingi 1,200 kwa pipa.

Miradi Inayoendelea na Uchumi

Rahma alisema kuna miradi mingine muhimu inayoendelea ikiwemo ujenzi wa stendi kuu ya Ibinzamata na barabara ya Mwawaza. Miradi hiyo ameitaja kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi katika Manispaa ya Shinyanga.

Ahadi za Siku 100 za Rais Samia Madarakani.

Rahma amenukuu baadhi ya vipaumbele  vya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba ndani ya siku 100 za mwanzo katika Urais wake, kwamba ataboresha sekta za elimu, afya, ajira, na kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya.

Akizungumzia ahadi za Rais Samia, Rahma Kware alitaja mipango miwili mikuu:

1.  Afya kwa Wote: Rais ameahidi kuzindua Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote, ambao utagharamia matibabu kwa makundi maalum kama vile wazee, watoto, mama wajawazito, na watu wenye ulemavu.

2.  Uwezeshaji Kiuchumi: Serikali imetenga Shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, bodaboda, mama lishe, na wajasiriamali wadogo kunufaika na huduma rasmi.

Wito kwa Wananchi wa Shinyanga

Rahma alihitimisha kwa maneno haya: "Waswahili wanasema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Katambi anatutosha"huku akitoa wito kwa Wanashinyanga kwenda kumshukuru Katambi kwa kumpa kura nyingi za kishindo ili arudi kuwatumikia tena kwa awamu nyingine, pamoja na ushindi mnono kwa Rais.Dkt Samia Suluhu Hassan.

 

 

 

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464