` CRDB YABORESHA HUDUMA ZA AFYA KAHAMA KUPITIA PROGRAMU YA EMPLOYEE VOLUNTEERING

CRDB YABORESHA HUDUMA ZA AFYA KAHAMA KUPITIA PROGRAMU YA EMPLOYEE VOLUNTEERING

 Katika kutekeleza Programu ya Employee Volunteering, wafanyakazi wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi jana wamekabidhi msaada wa vifaa vya hospitali vyenye thamani ya Shilingi milioni 17 kwa Hospitali ya Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga.

Msaada huo unajumuisha vitanda 20, magodoro 20, mashuka na foronya 100 pamoja na vifaa mbalimbali vya usafi.

Makabidhiano hayo yamefanyika Agosti 9,2025 katika viwanja vya hospitali hiyo, yakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa CRDB, Ndg. Matungwa Babyega, akiwa ameambatana na Meneja wa Kanda ya Magharibi, Ndg. Jumanne Wagana, pamoja na viongozi wengine kutoka makao makuu na ofisi za kanda.

Vifaa hivyo vimepokelewa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Yudas Ndungile, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. 

Akipokea msaada huo, Dkt. Ndungile ameishukuru Benki ya CRDB kwa mchango wao muhimu katika kuboresha huduma za afya, akisisitiza kuwa vifaa hivyo vitasaidia kupunguza changamoto ya upungufu wa vitanda na magodoro hospitalini hapo.


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464