` CCM YATANGAZA MATOKEO YA JIMBO LA KAHAMA, MSALALA & USHETU.

CCM YATANGAZA MATOKEO YA JIMBO LA KAHAMA, MSALALA & USHETU.




 Na Neema Sawaka

Katibu wa CCM wilaya ya Kahama Andrew Chatwanga ametaja  matokeo kwenye majimbo matatu  kwa nafasi za ubunge kwa majimbo matatu ya msalala,kahama na ushetu.Ambapo Msalala wagombea walikuwa sita na wajumbe 7845  na kura halali zilizopigwa 7685 na zilizohalibika ni 160.

Ambapo  Mabula  Magangila aliongoza nakupata kura 5518,Ambrose  Nangale  kura 929,Simon Lufyega kura 189, Ezeckiel Maige kura 791,Edson Masondole kura 152 na Emanuel Shiganza Kura 105.

Chatwanga amesema  waliopigiwa kura wajumbe  kwa Kahama mjini  walikuwa 6193 na kura 80 zilihalibika na halali kura ni  6113 ambapo  aliyeongoza  ni Benjamini  Ngaiwa alipata kura  2093, Sweetbert Nkuba  kura 1389, Jumanne Kishimba  kura 1144,

Francis Mihayo kura 821 na James Lembeli  kura 219, Juliana Kajala kura 256.

Chatwanga amesema  jimbo la Ushetu Emanuel Cherehani aliongoza  alipata kura 5656, Machibya Mwambilija  kura 171 ,Valerian  Mwambasha  alipata kura  153  Musa  Misungwi alipata kura 452 na zoezi la kupiga kura za maoni kata tatu kati ya 20 zilizopo ikiendelea.

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464