
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Ahmed Salum alikuwa anachuana na wagombea wengine sita akiwemo Sosthenes Julius Katwale aliyeshika nafasi ya pili kwa kupata kura 2,288, akifuatiwa na Selemani Emmanuel Chokala (kura 645), Zinguji Mayala Machwele (kura 67), Alphistone Michael Bushi (kura 61), Costantine Joseph Budaga (kura 59) na Leonard Nduta Lukanya aliyepata kura 30.
Akizungumza baada ya kutangaza matokeo hayo, Katibu wa CCM Wilaya ya Shinyanga Vijijini ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi, Erenestina Richard, amesema kuwa matokeo hayo ni ya awali, na uteuzi rasmi wa mgombea wa CCM bado unasubiriwa kupitia vikao vya juu vya uteuzi vya chama.
