
Alikuwa Mbabe wa Kucheat, Sasa Anaogopa Kuchati Na Shamba Girl
Kabla sijajua nini maana ya amani ya ndoa, nilijua uchungu wa usaliti. Mume wangu alikuwa mwanaume wa heshima mbele za watu, lakini ndani ya nyumba aligeuka kuwa mtu tofauti kabisa. Simu yake ilikuwa kama kifaru haiwezi kuguswa, kuangaliwa wala kuulizwa. Usiku wa manane alikuwa akiandika meseji kwa kucheka kimya, mchana alikua akijifanya kazini, kumbe yuko na wake wa watu.
Nilijaribu kila njia ya kawaida kumrekebisha. Nilimkumbusha viapo vya ndoa, nilimletea wazee, hata nilijaribu kumfuatilia. Kila mara aligeuza makosa kuwa yangu. Alisema “wewe ndio hunielewi,” au “unahisi tu.” Lakini mara kwa mara, nilipata meseji chafu, sauti za mapenzi, na hata picha zisizofaa kwenye simu yake.