` WAENDESHA BODABODA SHINYANGA WAPATA ELIMU YA VIPIMO

WAENDESHA BODABODA SHINYANGA WAPATA ELIMU YA VIPIMO

 

Afisa wa ofisi ya wakala wa vipimo mkoa wa Shinyanga, Leo Patrick akitoa elimu katika kituo cha uzaji wa mafuta kwa vyombo vya usafiri juu ya umuhimu wa kutambua vipimo katika kuadhimisha siku ya vipimo duniani.

Na Kareny  Masasy,

Shinyanga

WAKALA wa Vipimo mkoa wa Shinyanga (WMA) umetoa elimu kwa baadhi ya waendesha bodaboda  kwaajili ya kuthibiti Vipimo kwenye vituo vya utolea huduma ya mafuta ili kujua hali halisi ya Vipimo wanavyovipata kama ni sahihi.

Hayo yamesemwa leo mei 20,2025 na Ofisa Vipimo,  Leo Patrick  katika kuadhimisha siku ya vipimo duniani iliyoendana na utowaji wa elimu  na namna ya kutambuzi wa  pampu yenye  stika  ya Wakala ya  Vipimo   iliyothibitishwa kwa matumizi halali ya utoaji huduma na yenye kipimo halali.

 Patrick amesema  kauli mbiu ya mwaka huu ni  vipimo kwa Watu wote na Muda wote ikiwa utoaji wa elimu hii  lengo lake ni kubaini pampu hizo kama zinatumika kwa kuendana na uhalisi wa Vipimo kama inavyohitajika.

“Elimu leo tumeitoa ili kuweza kuthibiti wimbi la wizi kwa watumiaji kwani dhima ya Wakala wa Vipimo ni kuhakikisha mlaji au mtumiaji anakuwa  kwenye hali ya  Usalama,afya,kibiashara  na Mazingira” amesema Patrick.

Patrick amesema utoaji wa elimu kwenye vituo vya mafuta  ni moja ya eneo linalohusika na  Wakala wa Vipimo kwa kuthibitisha  kuwa  Vipimo ni sahihi  ikiwa maeneo mengi wamekuwa wakihusika katika kutoa elimu na kuthibiti kupunja walaji.

Ofisa Vipimo Baraka Mbizo amesema  leo ni siku ya vipimo duniani na  wametembelea   kituo cha mafuta na kuna stika iliyopo kwenye mashine inaonyesha  ilikaguliwa lini na mwisho wa matumizi ya pampu ni lini.

Mbizo amesema  muda wowote wamekuwa wakifanya ukaguzi wa kushtukiza  na wamekuwa wakitoa elimu mara kwa mara na kuhakikisha pampu inakuwa inaanzia namba sifuri  bila kuingiliana na mteja mwingine.

Mbizo amesema pindi wakipata malalamiko   kuwa kituo fulani kinafanya udanganyifu  na uchunguzi ukafanyika  na kubainika kuwa kweli hatua za kisheria zitachukuliwa kwa mujibu wa  sheria za Wakala wa Vipimo za  mwaka 2002  kwa  kutozwa faini .

Mbizo amesema   faini hizo zinazotozwa kwa mujibu wa sheria  pindi  mmiliki akikutwa na  makosa ambapo itatozwa  shilingi milioni 3 hadi tano au kifungo  cha   miaka mitatu kwenda jela.

 Mwenyekiti wa kituo cha bodaboda  mtaa wa ushirika,Frank Mahende alipongeza wakala wa vipimo kwa elimu waliyoitoa  kujua stika iliyowekwa ina umuhimu wa kujua  uhalali wa vipimo kwenye mafuta wanaoupata  kutokana na safari wanazozunguka.

Mwendesha bodaboda Hamis  Mshandete mkazi wa  ushirika manispaa ya Shinyanga  amesema Wakala wa Vipimo wametoa elimu na   amejifunza namna ya uwepo wa  stika zilizo kwenye  mashine  ili kuweza kupata mafuta  kupitia  Vipimo halali.





Muuzaji wa sheli,maafisa wa ofisi ya vipimo na madereva boda boda wakifatilia elimu ya vipimo.

 


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464