“Si uliniambia umeenda Dar?”. Ndivyo alivyoniuliza mke wangu, sauti yake ilisikika usiku wa manane wenye kimya kingi. Mimi, Eric, nilikuwa nikishuku uaminifu wa mke wangu katika ndoa yetu kwa muda mrefu.

Nakumbuka tulikuwa tumefunga ndoa ya kanisani, tumefungwa na viapo vitakatifu, lakini sikuweza kuondoa shaka kwamba alikuwa akiwatamani wanaume wengine huko nje.