
Walinifukuza Kazini Kwa Kusema Sina Malengo, Leo Mimi Ndiye Ninawaajiri Watoto Wao
Sikuwahi kusahau siku ile waliyoniita ofisi walinifukuza, na meneja wa kampuni niliyokuwa nafanya kazi kama msaidizi wa ghala. Alikuwa na uso wa baridi, na maneno yake yalikuwa makali kana kwamba alikuwa amenitayarishia hukumu ya maisha.
“Hatuoni kama una malengo ya kweli ya maisha. Unaonekana kama mtu asiyejitambua. Hii kazi si yako,” alinambia mbele ya wenzangu. Hakuna aliyenitetea. Niliondoka nikiwa nimevunjika moyo, nikijiona sifai.