Mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi aachiwa huru Tanzania - Hussein Khalid

Mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi ameachiliwa huru na Tanzania, mkurugenzi mtendaji wa shirika la Haki Afrika aliiambia BBC.
Waziri Mkuu na Katibu wa Baraza la Mawaziri Musalia Mudavadi, awali alikuwa pia ametangaza kuachiliwa kwa mwanaharakati huyo ambaye alikuwa amekamatwa nchini Tanzania kwa siku kadhaa.