Header Ads Widget

WADAU SHINYANGA WAIPOKEA PJT -MMMAM WATAKA IPEWE KIPAUMBELE



 Ofisa  Maendeleo ya jamii Tedson Ngwale.

Na Kareny Masasy,Shinyanga

WADAU zaidi ya 150  mkoani Shinyanga wamepokea program  Jumuishi  ya Taifa  ya Malezi,Makuzi na Maendeleo  ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) huku wakielezwa sayansi ya makuzi inayoambatana  katika nguzo tano za lishe,ulinzi na usalama, ,afya,malezi yenye mwitikio na ujifunzaji wa awali.

Wadau hao  leo tarehe 20/09/2023 baada ya kushiriki  uzinduzi wa programu hiyo mkoani Shinyanga   wamepewa elimu juu ya sayansi ya Makuzi na Malezi ya mtoto kutoka kwa mtaalamu  Andrew  Nkunga anayetokea kwenye Mtandao wa malezi na Makuzi ya Mtoto nchini  (TECDEN).

Nkunga akitoa elimu hiyo amesema mtoto hatua za makuzi  zinaanzia umri wa 0 hadi miaka nane ni kipindi ambacho mtoto ubongo  unaanza kukua  ikiwa atapata changamoto kwenye ukuaji hata ukuaji wake hautakuwa timilifu.

“Ubongo lazima ukue vizuri ili vitu vyote viende sawa na taarifa kupitia kwa mtoto kabla ya kuzaliwa na baada ya kuzaliwa  hutumia milango ya fahamu  na kupeleka kwenye ubongo  hivyo wazazi na walezi wanashauriwa kutowatendea vitendo vya ukatili watoto,kuwatukana kuwafokea”amesema Nkunga.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa  mkuu wa wilaya ya Kishapu  Joseph Mkude kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga  Christina Mndeme amesema amepongeza wadau walioshiriki   program jumuishi  ikiwa inahitaji kupewa kipaumbele  na watoto wote wawe katika ukuaji timilifu.

“Tumeelezwa hapa duniani  kuna watoto taribani Millioni 250 wenye umri  chini ya miaka  mitano  ambao wanapatikana  kwenye nchi za uchumi wa kati  na  uchumi wa chini  hivyo ni jukumu letu sote kuwalinda watoto ili wasipatwe na vitendo vya ukatili na kukua kwa utimilifu”.amesema mkude.

Afisa Maendeleo ya jamii  mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale  amesema taasisi zinazolea watoto  ndani ya mkoa zinapatiwa mafunzo sababu zimekuwa zikiishi na watoto  wenye umri  mdogo kwa kusaidia wazazi wao   ili watoto hao wawe katika  msingi bora ambapo elimu inayotolewa sasa ni  fursa  ya namna ya kuwalea watoto ili kupata taifa imara.

Akitambulisha program hiyo  kwa niaba ya  mkurugenzi wa  shirika la  ICS  Sabrina  Majikata amesema kwanini  wanazungumzia  kuhusu umri  wa miaka 0 hadi nane ni kumjenga mtoto katika ukuaji wake.

Majikata amesema mtoto  akiwa bado mdogo  ubongo unahitaji kujijenga zaidi  na kunatakiwa kutiliwe mkazo katika nguzo tano  za lishe,afyabora,Malezi yenye mwitikio,ujifunzaji wa awali na ulinzi na usalama.

“Serikali ilianza mchakato wa malezi na makuzi  tangu mwaka 2004 na mwaka 2006 ilifanya mapatio ya sera ya mtoto  na imeanza  kupitiwa  upya na viongozi hapa nchini  kupitia sekta mbalimbali wametoa ahadi ya kutekeleza  mchakato  na sasa  umeanza utekelezaji wake ili kumkomboa mtoto”amesema Majikata.

Majikata amesema shirika la watoto duniani  (Unicef ) na  shirika la afya duniani (WHO) lilitengeneza framu  ya nguzo tano  hizo kuhakikisha wanawekeza katika umri wa miaka mitatu lakini  taifa  la Tanzania liliangalia hilo nakuona kuwekeza katika  umri wa mwaka 0 hadi nane.

 “Wataalamu wanasema ukiwekeza katika umri mdogo ndiyo utaweza kumsadia mtoto katika ukuaji wake kwenye  ubongo  na sio kuwekeza katika umri mkubwa ubongo umekwisha komaa”anasema Majikata.

Mwakilishi  wa meneja wa kanda ya ziwa kutoka Shirika la kimataifa la Word division  Ngasa Michael  amesema wanagusa watoto kupitia nguzo nne za ustawi wa mtoto ambao ni Afya, Elimu,Malezi na  ulinzi na usalama kuhakikisha  mtoto anakuwa katika ustawi ulio bora.

 ,K


Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto mkoani Shinyanga akijitambulisha kwenye uzinduzi.

Wadau wakisikiliza  mada ya elimu juu ya sayansi ya makuzi kwa mtoto.


Mtaalamu kutoka TECDEN  andrew Nkunga akijitambulisha kwa wadau mkoani Shinyanga.

Mwakilishi wa shirika la ICS Sabrina Majikata akijitambulisha




Mwakilishi wa shirika la Doctors with Afrika akifuatilia mada.

Wadau wakifuatilia mada inayofundishwa baada ya uzinduzi wa programu jumuishi .



Wadau wakifuatilia   elimu inayotolewa juu ya makuzi,maendeleo ya awali ya mtoto  na  malezi ya watoto



Mratibu wa WFT kutoka Shinyanga  Gloria Mbia akijitambulisha kwa wadau wengine katika uzinduzi







Wadau wakisikiliza  mada.






Post a Comment

0 Comments