Header Ads Widget

NONDO NNE ZA CHADEMA MWAKA 2025


Hizi hapa nondo nne za Chadema 2025

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe

Mwanza.Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezindua kampeni yake ya operesheni ‘+255 Katiba Mpya Okoa Bandari Zetu’ mjini Bukoba Julai 28, 2023, kikiainisha hoja itakazonadi kwa Watanzania kupitia mikutano yake ya hadhara, ikiwa pamoja na mabadiliko ya Katiba kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.


Wakiongozwa na Mwenyekiti, Freeman Mbowe, viongozi wa Chadema waliohutubia mkutano uliofanyika Uwanja wa Uhuru maarufu kama uwanja wa Mayunga mjini Bukoba, walitaja madai ya Katiba mpya, mkataba wa uwekezaji bandarini, hali ya wananchi na Taifa kiuchumi na matumizi ya rasilimali za Taifa kuwa ajenda kuu za operesheni hiyo itakayosambaa kote nchini.

Akihutubia mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika alisisitiza msimamo wa chama hicho wa kupatikana Katiba mpya kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, ili kuweka mazingira sawa ya kushindana kisiasa kwa vyama vyote.

SOMA HAPA ZAIDI CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments