Header Ads Widget

WATU WAWILI WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA AJALI BASI LA KILIMANJARO EXPRESS, GARI DOGO


Watu wawili wanahofiwa kufa katika ajali iliyohusisha basi la Kilimanjaro Express lililokuwa likitokea Arusha kwenda Dar es Salaam kugongana na gari dogo katika Kijiji cha Kijomu, kilichopo kata ya Hedaru wilayani Same Mkoani Kilimanjaro.


Kwa mujibu wa Mtendaji wa kijiji cha Kijomu Veran Mtenga amesema ajali hiyo imetokea leo Juni 23, 2023 saa 12 asubuhi likihusisha basi la Kilimanjaro na gari dogo ambalo lilikuwa limeharibika ambapo kwenye gari dogo kulikuwa na watu miwili, mwanamke na mwanaume.

Post a Comment

0 Comments