Header Ads Widget

WANANCHI WAIPONGEZA TANESCO KUCHUKUA HATUA ZA HARAKA KUREJESHA UMEME, KUDHIBITI ATHARI ZAIDI MVUA YA UPEPO SHINYANGA


Mafundi wa TANESCO wakiendelea na kazi ya kutengeneza miundombinu ya umeme katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 


Na Halima Khoya - Shinyanga

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga wamelishukuru Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Shinyanga kwa jitihada wanazozifanya kurejesha huduma hiyo mara baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha February 2,2023 hali iliyosababisha uharibifu wa miundombinu ya umeme pamoja na nyumba kuanguka.


Wananchi hao wametoa Pongezi leo February,03,2023 wakati Wafanyakazi wa TANESCO wakiendelea na  zoezi la kurekebisha miundombinu ya umeme maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Shinyanga  yaliyoathiriwa na mvua hiyo ya upepo.

Saidi Hussein na Josephina Mondi ni miongoni mwa wateja wa TANESCO walioathiriwa na mvua ambapo wamesema ulianza upepo kisha wakasikia mtikisiko mkubwa ambao umesababisha kuanguka kwa nguzo ya umeme  na nyumba kubomoka.

Aidha wameishukuru TANESCO kuchukua hatua za haraka kuzima umeme mapema hali iliyosababisha kutokuwepo kwa madhara kwa binadamu.

Kaimu Meneja  wa TANESCO mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Leo Mwakatobe, amesema kuwa mvua hiyo imesababisha madhara ya kuanguka kwa nguzo maeneo mbal mbali katika Manispaa hiyo hali iliyosababisha wateja wao kukosa huduma ya umeme lakini pia shirika hilo kukosa mapato kwa kusambaza umeme.


Mwakatobe amesema wateja wengi wamerejeshewa huduma ya umeme na  wanaendelea kurejesha umeme kwenye maeneo yaliyobakia  huku akiwaasa wananchi waendelee kutoa taarifa mapema inapotokea changamoto ya umeme ili kitengo cha dharura kiwajibike haraka na kuondokana na madhara makubwa.


"Sisi shirika la umeme tumepata athari kubwa nguzo nyingi zimedondoka, wateja wengine mita zao zimevunjika baada ya kuangukiwa na miti kwa hiyo shirika limekosa mapato. Licha ya kutokea kwa changamoto hiyo TANESCO Shinyanga kitengo chetu cha dharura kimesimama vyema na hakuna athari iliyotokea kwa binadamu zaidi ya baadhi ya nyumba za wateja wetu kuharibika" amesema Mhandisi Mwakatobe.
Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe akionesha nguzo za umeme zilizoanguka katika eneo la Nhelegani Manispaa ya Shinyanga kufuatia mvua iliyoambatana na upepo Februari 2,2023.  Picha na Kadama Malunde
Zoezi la kuchimba mashimo kwa ajili ya kuweka nguzo mpya za umeme likiendelea katika eneo la Nhelegani Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa Nguzo za umeme zilizoathiriwa na Mvua ya upepo katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 
Muonekano wa Nguzo za umeme zilizoathiriwa na Mvua ya upepo katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 
Fundi wa TANESCO akiendelea na kazi ya kutengeneza miundombinu ya umeme katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 
Fundi wa TANESCO akiendelea na kazi ya kutengeneza miundombinu ya umeme katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 
Mafundi wa TANESCO wakiendelea na kazi ya kutengeneza miundombinu ya umeme katika eneo  la Iwelyangula kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga 

Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe (katikati), Mhandisi Mkuu wa TANESCO Shinyanga, Kurwa Mangara (kulia)  na Afisa Mahusiano na Huduma kwa wateja Lilian Mungai wakiangalia nguzo ya umeme iliyoathiriwa na mvua ya upepo kwenye nyumba ya mteja wa TANESCO eneo la Buhangija Mjini Shinyanga
Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe akionesha miundombinu ya umeme iliyoharibika kufuatia mvua ya upepo kuangusha mti katika eneo la Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga
Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe akionesha miundombinu ya umeme iliyoharibika kufuatia mvua ya upepo kuangusha mti katika eneo la Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga
Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe akionesha miundombinu ya umeme iliyoharibika kufuatia mvua ya upepo kuangusha mti katika eneo la Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Mchungaji wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga, Daniel Emmanuel Manga akielezea jinsi mvua ya upepo ilivyoharibu kanisa hilo.
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Muonekano wa Kanisa la EAGT Mshikamano kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga lililoanguka kufuatia mvua ya upepo iliyonyesha Februari 2,2023
Mhandisi Mkuu wa TANESCO Shinyanga, Kurwa Mangara akionesha  mita na chuma cha kupokelea umeme kutoka kwenye nguzo kwenda kwenye nyumba ya mkazi wa Lubaga Mjini Shinyanga baada ya kuathiriwa na mvua ya upepo. Kushoto ni Afisa Mahusiano na Huduma kwa wateja Lilian Mungai katikati ni Kaimu Meneja TANESCO Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Leo Mwakatobe
Zeozi la kurejesha huduma ya umeme likiendelea katika eneo la Lubaga Mjini Shinyanga 
Zeozi la kurejesha huduma ya umeme likiendelea katika eneo la Lubaga Mjini Shinyanga .

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Post a Comment

0 Comments