Header Ads Widget

WIKI YA SHERIA YAZINDULIWA SHINYANGA, WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA KUPATA ELIMU NA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA BURE


Uzinduzi Maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

WANANCHI wa Mkoa wa Shinyanga, wametakiwa kutumia fursa madhimisho ya wiki ya sheria, kujitokeza kwa wingi kupata elimu ya sheria na msaada wa kisheria bure, ili kufahamu namna ya kupata haki zao kwa mujibu wa sheria.


Maadhimisho hayo ya Sheria hapa nchini yameanza leo Januari 22 na yatahitimishwa Februari 1 mwaka huu, ambapo katika Mkoa wa Shinyanga kutakuwa na utoaji wa elimu ya sheria na kupatiwa msaada wa kisheria bure, na usikilizwaji  kero mbalimbali na kutafutiwa ufumbuzi, ambayo itakuwa ikitolewa katika viwanja vya Zimamoto vilivyopo Nguzonane Manispaa ya Shinyanga.

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude, ametoa wito huo wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga kwa niaba ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Yahaya Nawanda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, amewataka wananchi wa Mkoa wa Shinyanga watumie fursa kwenye maadhimisho hayo ya wiki ya Sheria kupata elimu na msaada wa kisheria bure pamoja na kupata ufumbuzi wa matatizo yao.

Katika hatua nyingine Mkude amewataka wananchi wanapokuwa na matatizo ya migogoro, wasikimbile tu mahakamani, bali waitatue kwa njia ya usuluhishi na kuleta amani, pamoja na kutopoteza muda kwa kufanya shughuli za uzalishaji kwa kuhudhuria mahakamani kila mara.

Alitoa wito pia kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga, wajitokeze kwa wingi kwenye mabanda katika wiki hiyo ya Sheria, ili wapate elimu mbalimbali za msaada wa kisheria, na kupata haki zao kwa mujibu wa Sheria.

Aidha, aliwataka watumishi wa mahakama kufanya kazi zao kwa weledi, kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, sheria, kanuni na miongozo ya Serikali kwa watumishi wa umma, ili kutoa haki sawa kwa wananchi katika utatuzi wa migogoro yao.

“Natoa Rai kwa wananchi kila wanapokuwa na migogoro wasikimbile Mahakamani, bali waitatue kwa njia ya usuluhishi na kuleta amani, na ile ambayo itashindikana ndipo waipeleke mahakamani,” alisema Mkude.

“Natoa Rai kwa wananchi kila wanapokuwa na migogoro wasikimbile Mahakamani, bali waitatue kwa njia ya usuluhishi na kuleta amani, na ile ambayo itashindikana ndipo waipeleke mahakamani,” amesema Mkude.

Aidha, amewataka watumishi wa mahakama kufanya kazi zao kwa weledi, kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, sheria, kanuni na miongozo ya Serikali kwa watumishi wa umma, ili kutoa haki sawa kwa wananchi katika utatuzi wa migogoro yao.

Naye Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Athumani Matuma, alikazia suala la utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi, na kueleza kuwa ni njia ambayo itapunguza pia mrundikano wa kesi mahakamani, sababu kuna kesi nyingine siyo za kupelekwa mahakamani bali zinahitaji usuluhishi.

Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya wiki ya Sheria inasema, umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu wajibu wa mahakama na wadau.


Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Athumani Matuma akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Athumani Matuma, (kushoto) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Uzinduzi maadhimisho ya wiki ya Sheria mkoani Shinyanga yakiendelea.

Picha za pamoja zikipigwa kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Picha za pamoja zikipigwa kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.
Picha za pamoja zikipigwa kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.
Maandamano yakiendelea kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Maandamano yakiendelea kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Maandamano yakiendelea kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Maandamano yakiendelea kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Maandamano yakiendelea kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria mkoani Shinyanga.

Post a Comment

0 Comments