Header Ads Widget

KATAMBI AZINDUA MIRADI YA KIUCHUMI MANISPAA YA SHINYANGA, APONGEZA UTOAJI MIKOPO MIRADI YENYE TIJA


Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu akiendesha gari dogo aina ya Coaster ambayo wamepewa mkopo vijana, kikundi cha vijana wabunifu kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga asilimia 10.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA .

MBUNGE wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, amezindua miradi ya kiuchumi Manispaa ya Shinyanga, huku akipongeza utoaji wa fedha za mikopo kwenye miradi yenye tija ambayo itawainua wananchi kiuchumi.
 
Uzinduzi huo umefanyika leo Desemba 18, 2022 na kuhudhuliwa na mamia ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga, watumishi wa Serikali, madiwani na viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Miradi ya kiuchumi ambayo imezinduliwa ni kituo cha Urasimishaji, Ewekezaji, na uendelezaji wa biashara, Soko la Machinga, pamoja na kukabidhi gari dogo aina ya Coaster ambalo wamepewa vijana mkopo Sh.milioni 60 kupitia mapato ya ndani asilimia 10.

Katambi ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akizungumza kwenye uzinduzi wa miradi hiyo ya kiuchumi, amepongeza uongozi wa Manispaa ya Shinyanga, watumishi pamoja na madiwani kwa usimamizi mzuri wa fedha za mapato na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Amesema Chama cha Mapinduzi (CCM)­ kikiahidi jambo lazima kitekeleze, na sasa wananchi wameanza kujionea wenyewe matunda ya CCM, ambapo miradi mingi ya maendeleo inatekelezwa pamoja na kutatua kero ambazo zinawakabili na kuwanyanyua kiuchumi.

“Shinyanga sasa hivi inapaa kimaendeleo na sisi kama viongozi tutaendelea kushirikiana pamoja, ili kuhakikisha mji wa Shinyanga una kwenda kwenye hadhi ya Jiji,”amesema Katambi.

“Napongeza pia kwa utoaji wa fedha za mikopo asilimia 10, na fedha hizi zinawafikia walengwa, na hii ndiyo Adhima ya Rais Samia kuwa fedha hizi zinufaishe watu husika na kuwanyanyua kiuchumi, natoa wito kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu nendeni mkakope fedha zipo na hazina riba,”ameongeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, amesema kazi ya Serikali ni kuboresha mazingira ya kibiashara kwa wananchi, na ndiyo maana wameanza kuimarisha huduma hizo za kiuchumi ikiwamo ujenzi wa Masoko, Stendi za Mabasi, kuboresha kituo cha Urasimishaji, Ewekezaji na uendelezaji wa biashara na utoaji wa mikopo.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akizungumza kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anold Makombe akizungumza kwenye uzinduzi wa mirad ya kiuchumi.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Ester Makune akizungumza kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura akielezea namna Serikali inavyoboresha ustawi wa maisha ya wananchi kiuchumi.
Afisa Biashara wa Manispaa ya Shinyanga Milembe George akisoma taarifa ya ukarabati wa kituo cha Urasimishaji, ewekezaji na uendelezaji wa biashara.

Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga John Tesha, akitoa taarifa ya utoaji mkopo basi dogo la vijana Sh,milioni 60.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akikata utepe akizindua kituo cha Urasimishaji, Ewekezaji na Uendelezaji wa biashara.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akikata utepe akizindua kituo cha Urasimishaji, Ewekezaji na Uendelezaji wa biashara.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akikata utepe kwenye gari la mkopo la vijana.
Muonekano wa gari aina ya Coaster ambayo wamepewa mkopo vijana, kikundi cha vijana wabunifu kupitia fedha za mapato ya ndani asilimia 10.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akiendesha gari ambalo wamepwa mkopo vijana.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, akiendesha gari ambalo wamepwa mkopo vijana.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu,akikata Utepe kuzindua Soko la Machinga.

Muonekano wa Soko la Machinga.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu,akipanda Mti katika Soko la Machinga.

Viongozi wakiwa meza kuu kwenye uzinduzi wa mirad ya kiuchumi.

Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga pamoja na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Madiwani, viongozi wa CCM pamoja na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Uzinduzi wa miradi ya kiuchumi ikiendelea.

Uzinduzi wa miradi ya kiuchumi ikiendelea.

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Uzinduzi wa miradi ya kiuchumi ikiendelea.

Uzinduzi wa miradi ya kiuchumi ikiendelea.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu (katikati) akikagua ujenzi wa Soko kuu la Manispaa ya Shinyanga, hadhi ya Ghorofa.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura kwenye ujenzi wa Soko Kuu la Manispaa ya Shinyanga wakiteta jambo.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana Ajira na watu wenye ulemavu, awali wakiwasili kwenye uzinduzi wa miradi ya kiuchumi.

Post a Comment

0 Comments