Header Ads Widget

YANGA SC YAICHAPA TANZANIA PRISONS 1-0 DAKIKA ZA LALA SALAMA






****************


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM


KLABU ya Yanga imeichapa timu ya Tanzania Prison 1-0, bao lililofungwa na Feisal Salum dakika za lala salama na kuifanya timu yake kuondoka na alama tatu kwenye mchezo huo ambao uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa.

Tanzania Prison kipindi cha kwanza waliweza kukamatwa kwani walikuwa wanashambuliwa huku wakiweza kuzuia nafasi nyingi ambazo zilikuwa zinatengenezwa na Yanga Sc.


Kipindi cha pili Yanga Sc ilifanya mabadiliko ya baadhi ya mastaa wao akiwemo Dickson Ambundo, Kibwana Shomari na Clement Mzize mabadiliko ambayo yalizaa matunda.


Yanga Sc iliwakosa baadhi ya mastaa wao kwa sababu mbalimbali ambapo Fiston Mayele, Bakari Nondo wakisumbuliwa na majeraha.

Post a Comment

0 Comments