Header Ads Widget

PROFESA MAHALU BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO NA KIFUA AMESEMA WAZAZI WENGI HAWATAMBUI CHANZO CHA MAGONJWA YA MOYO KWA WATOTO WAO



PROFESA  Williamu Mahalu  ambaye ni bingwa mbobezi wa  upasuaji wa moyo na  kifua  kutoka Hospitali ya  rufaa Bugando.  

Na Kareny  Masasy, Bukombe

PROFESA  Williamu Mahalu  ambaye ni bingwa mbobezi wa  upasuaji wa moyo na  kifua  kutoka Hospitali ya  rufaa Bugando  amesema wazazi wengi hawatambui matatizo ya moyo kwa watoto wao.

Na  kati ya watoto laki moja  basi  watoto 15 wanakutwa na magonjwa ya moyo hapa nchini.

Profesa Mahalu amesema hayo jana  mbele ya waandishi wa habari  katika hospitali  ya  binafsi ya Charles Kulwa Memorial iliyopo Ruzewe wilayani Bukombe mkoani Geita  ambapo amekuwa akitoa huduma ya kutibu Moyo  kwa watu wazima na watoto.

Profesa Mahalu  amesema   wazazi wengi hawatambui matatizo ya moyo kwa watoto wao kwani hospitalini hapo amekuwa akiwatibu watu wengi  kwa mwezi  wagonjwa  wenye matatizo ya moyo ni  77 hadi 80   kati yao watoto ni asilimia 5.

“Wazazi wengi hawatambui  magonjwa  ya moyo kwa watoto wao wengi wanafikiri mtoto anakikohozi nakumpeleka kwenye vituo vya afya au zahanati hawafikirii kuwapatia vipimo ili kubaini tatizo mapema”alisema profess Mahalu.

Profesa  Mahalu amesema  magonjwa ya kuridhi  mfano shinikizo la damu  mengine yakuyapata  kutokana  na desturi ya vyakula vinavyoliwa kwa  kuwekewa mafuta mengi  nakufanya moyo kutanuka na wengine kuzaliwa  moyo na matundu.

“Zamani walikuwa na imani za kishirikina lakini sio kwamba siku hizi magonjwa mengi bali yametambuliwa  mengi na kufanyiwa mchakato wa kupata tiba yake”amesema  profesa Mahalu.

Profesa Mahalu amesema   bado watu wanatumia ulaji wa chumvi  usio na utaratibu  mzuri nao ni changamoto inayoleta madhara katika moyo ushauri waepuke ili kuondoa madhara hayo.

‘Wagonjwa wengi walikuwa wakishindwa kusafiri kwenda Mwanza kupata matibabu ya Moyo  lakini hospitali ya Charles Kulwa Memorial  imeweza kusogeza huduma hii kwa ukaribu.”amesema  profesa Mahalu.

Mkurugenzi wa hospitali ya Charles  Kulwa Memorial  dkt  Baraka Kulwa  anasema  kwa sasa  wamekuwa wakitoa  huduma za kibingwa  kila siku na madaktari wapo zamani ilikuwa mara moja kwa mwezi.

Kulwa anasema wagonjwa wamekuwa wakiongezeka kutoka maeneo mbalimbali wenye bima za afya  na wasiokuwa nazo  kwani kiwango wanachokitoa ni kama hospitali ya wilaya na sasa wanataka kupigania ifike kiwango cha mkoa.

Dkt Kulwa amesema  serikali imeweka mazingira mazuri kwa ushirikiano wa kutoa baadhi ya dawa na vifaa tiba bure kwa lengo la kutoa huduma ya kliniki  kwa baba,mama na mtoto.

Baadhi ya magonjwa dawa zake tunapewa bure na serikali mojawapo ni kifua kikuu,  ukoma ,huduma za CTC  na huduma ya kliniki ya baba na mtoto (RCH) bure kwani vifaa tiba serikali inatoa ili kuokoa vifo vya mama na mtoto pia .

Mtaalamu wa  masuala ya mionzi (Utralsaound)  kutoka hospitali ya Charles Kulwa Memorial  Elmil  Mmanyi anawashauri   wajawazito   mimba inapofikisha  umri  wa miezi 20  wapate kuchunguzwa waangaliwe  vinasaba vya  mtoto kuzuia asipatwe na  matatizo ya mdomo sungura,kichwa kikubwa,moyo  na mgongo wazi .

Mmanyi amesema  wapo wajawazito waliofika hapo na kubainika watoto wao waliopo tumboni wana changamoto lakini  ilivyobainika  walianza kupata huduma na tatizo hilo likaondoka.

Mtaalamu wa Mionzi  bingwa kutoka hospiatli ya rufaa Bugando  Rajabu  Kidenda  anayetoa huduma kwenye hospitali ya Charles Kulwa Memorial anasema kuwa Utralsound ni mionzi iliyosalama  .

 Pia kwa siku katika hospitali hiyo huwafanyia watu 30 hadi 40 wakiwemo wajawazito  na wiki moja hutoa elimu mara mbili juu  mionzi hiyo.

Mtaalamu wa dawa za usingizi  dk Francs Mtola akiwa kwenye chumba cha upasuaji katika hospitali ya Charles Kulwa  Memorial
Mtaalamu kutoka kitendo cha upasuaji dk Danny  Maleka kutoka hospitali ya Charles Kulwa Memorial.
Eneo la Hospitali  ya  Charles Kulwa Memorial
eneo la chumba cha upasuaji katika hospitali ya Charles Kulwa  Memorial
Mtaalamu wa meno katika hospitali  ya Charles Kulwa akiwa kazini

 Mtaalamu wa maabara Yusuph Hashimu akiwa kazini katika hospitali ya Charles Kulwa  Memorial



Mtaalamu wa mionzi katika hospitali ya  Charles Kulwa Memorial akiwa kazini kutoka huduma.
Profesa Williamu Mahalu ambaye ni bingwa wa magonywa ya moyo na kifua kitoka hospitali ya rufaa ya Bugando ambaye amekuja kutoa huduma  za kibingwa katika hospitali ya Charles Kulwa Memorial 
Mkurugenzi wa hospitali ya Charles Kulwa Memorial  dkt Baraka Kulwa akiwa kwenye chumba tayari kutoa huduma.

 Mtaalamu wa mionzi (ultrasound) kutoka hospitali ya rufaa ya Bugando  Rajabu Kidenda akiwa katika hospitali ya Charles Kulwa Memoriali akitoa huduma.

Post a Comment

0 Comments