Header Ads Widget

WATAALAMU WAELEZA SABABU KUWEPO KWA MAADHIMISHO SIKU YA KUNYWA BIA

Sababu kuwepo siku ya bia duniani
Wakati ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Bia leo, wataalamu wameeleza kinywaji hicho kinapewa umuhimu kwa sababu ya kuwaunganisha watu katika jamii, hasa maeneo yenye changamoto za kiusalama. 
Siku hiyo huadhimishwa kila Ijumaa ya kwanza ya Agosti na lengo lake ni kufurahia kinywaji hicho.

Bia ni kinywaji kinachopendwa na wengi na kina historia ndefu katika jamii tofauti na wamekuwa wakitumia kinywaji hicho kukaa pamoja na kujadiliana masuala mbalimbali au kufurahi pamoja katika matukio ya kijamii.

Ushahidi wa kale unaonyesha kwamba binadamu alianza kutengeneza bia katika miji ya Babylonia na Misopotania. Wataalamu wa historia wanabainisha kwamba viungo vya bia viliandikwa mwaka 4300 K.K.

Hata hivyo, siku hiyo ilianzia huko California, Agosti 2007 kabla ya kusambaa maeneo mengine duniani na malengo makuu yalikuwa ni kukusanyika na marafiki na kufurahia ladha ya bia, kusherehekea wanaotengeneza na kuhudumia bia na kuunganisha ulimwengu wote kupitia bia.
SOMA HAPA ZAIDI CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments