Header Ads Widget

UPINZANI WAGEUZWA MAFICHO YA WANACCM

Upinzani wageuzwa maficho ya wana CCM

Inaelekea kutimia miaka 30 tangu mfumo wa vyama vingi vya siasa urejeshwe mwaka 1992. Na iliigharimu nchi miaka 30 chini ya chama kimoja, mwaka 1962 mpaka 1992.

Vinara wa mageuzi waliokuwepo mwaka 1992 hawapo tena. Kuna waliochukuliwa na Mungu, wapo waliopumzika kwa sababu za kiafya na umri.

Mabere Marando hayupo kwenye uso wa jamii kisiasa, Ringo Tenga, Ndimara Tegambwage, Prince Bagenda, si wanasiasa tena. Hata hivyo, kumbukumbu za historia ya mageuzi zinawatambulisha kama watu muhimu waliochochea kabla na waliopokea mageuzi kwa mikono miwili.

Christopher Mtikila, Chifu Abdallah Said Fundikira, Kasanga Tumbo na Kasela Bantu, Shaban Moore, Lifa Chipaka, James Mapalala, Wilfrem Mwakitwange, Seif Sharif, Mwesiga Baregu na wengine, wote ni marehemu. Ila walihusika kuasisi vyama tofauti vya upinzani mwaka 1992.

SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI

Post a Comment

0 Comments