Header Ads Widget

YANGA YATINGA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO LA AZAM KWA KUICHAPA SIMBA BAO 1-0 CCM KIRUMBA



Dakika 90 za Mchezo wa Watani wa jadi, Yanga na Simba zimemalizika kwa Timu ya Yanga kuitwanga Simba SC bao 1-0 katika Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza na kutinga moja kwa moja fainal katika kombe la Shirikisho la AZAM.


Dakika 45 za kipindi cha kwanza kwa watani wa jadi kutoana jasho zimekamilika na ubao ukiwa unasoma Yanga 1-0 Simba.


Dakika 15 za mwanzo ilikuwa ni msako kwa kila timu kutafuta bao la kuongoza ambapo hakukuwa na aliyeweza kuona lango la mpinzani.


Yanga ilibidi wasubiri mpaka dakika ya 25 huku mtupiaji akiwa ni Feisal Salum kwa shuti kali akiwa nje ya 18 likamshinda mlinda mlango namba mbili wa Simba, Beno Kakolanya.

Post a Comment

0 Comments