Header Ads Widget

WAZIRI NAPE AYAFUNGULIA MAGAZETI YA TANZANIA DAIMA, MAWIO, MSETO NA MWANAHALISI


WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, ametangaza Rasmi leo Februari 10,2020 kuyafungulia Magazeti Manne ambayo yalikuwa yamefungiwa pamoja na kukabidhi Lesseni, kwenye mkutano wake na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini. 
Magazeti ambayo yamefunguliwa ni Tanzania Daima, Mawio, Mseto na Mwanahalisi.
 
 "leo nitatoa leseni kwa magazeti manne yaliyokuwa yamefungiwa ambayo ni Mwanahalisi, Mawio, Mseto na Tanzania Daima, kwasababu ni vizuri kuondoka kwenye maneno tufanye vitendo, hivyo tuanze na ukurasa upya sasa mwenye maneno yake aseme mwenyewe, kifungo kimetosha kikubwa kazi iendelee,”alisema Waziri Nape Nnauye.
 
 
 
 
 

Post a Comment

0 Comments