Header Ads Widget

WAZIRI MKUU DBEIBAH ANUSURIKA KIFO JARIBIO LA MAUAJI


Gali lililopigwa Risasi, halihusiani na tukio
 
Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid al-Dbeibah, amenusurika katika jaribio la mauaji lililofanywa na watu wasiojulikana.

Gari lake lilishambuliwa kwa risasi lilipokuwa likiendeshwa katika mji mkuu, Tripoli, mapema siku ya Alhamisi.

Watu wenye silaha walikimbia eneo la tukio.

Pande zinazozozana zimekuwa zikigombea udhibiti wa Libya, na bunge lenye makao yake mashariki mwa nchi hiyo litapiga kura baadaye siku ya Alhamisi kumchagua waziri mkuu atakayechukua nafasi ya serikali ya umoja wa kitaifa.

Bw Dbeibah amesema kuwa atapuuza matokeo ya kura hiyo.

Uchaguzi wa kuichagua serikali mpya uliahirishwa Disemba mwaka jana lakini hakuna kura inayotarajiwa mwaka huu

SOMA ZAIDI HAPA CHANZO BBC SWAHILI.


Post a Comment

0 Comments